Mabadiliko Mapya Katika Mfumo Wa Maswali Mitihani Ya Darasa La 7.


Afisa Habari wa Baraza la mitihani la Taifa (Necta), John Nchimbi amesema mabadiliko hayo katika mfumo wa utungaji wa mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi, aliyatangaza katibu Mkuu wa baraza hilo, Dkt. Charles Msonde katika mkutano mkuu wa tano wa maofisa elimu mkoa na wilaya unaofanyika mjini Dodoma, ambapo sasa kila somo litakuwa na maswali 45, kati ya hayo, maswali 40 yatakuwa ya kuchagua jibu sahihi na matano yatakuwa ya kujieleza/kuonyesha njia na jibu ili kupima uelewa wa wanafunzi watakaofanya mitihani hiyo.
Kwa maswali 40, kila moja litakuwa na alama 1 na maswali matano kila moja litakuwa na alama 2 huku majibu ya maswali 40 yatajibiwa kwenye fomu za OMR na maswali matano yatajibiwa kwenye karatasi maalum itakayoandaliwa.

 Aidha, Necta imetoa wito kwa walimu wakuu kuanza kuwapima wanafunzi kwa kutumia mabadiliko hayo ili kuwajengea uzoefu wasipate shida wakati wa mtihani huo wa Taifa.

Comments