JUMUIYA YA WAZAZI CCM-BUKOMBE YAIPONGEZA SERIKALI KUPUGUZA KWA CHANGAMOTO SHULE YA MSINGI NAMONGE

Wanachama wa chama cha mapinduzi CCM kupitia jumuiya ya wazazi Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita, wameipongeza serikali ya wamau ya tano kwa kupunguza changamoto zinazo ikabili shule ya msingi Namonge kata ya Namonge tarafa ya Siloka.
Wakati akipongeza jitihada za serikali  kwenye maadhisho ya jumuiya wa wazazi kiwilaya yaliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Namonge Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Jumuia ya Wazazi CCM Mkoa wa Geita John Kafimbi ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye madhimisho ya wiki ya jumuia ya wazazi CCM kufikisha umri wa miaka 63  huku  akichangia mifuko 10 ya saruji.
Mkuu wa Shule ya msingi Namonge Jemes Kadongo alisema shule hiyo iliazishwa mwaka 2002 na ina changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa kutokana na wingi wa wanafunzi kuazia darasa la awali hadi la saba ni wanafunzi 4,000 wasichana 1934 wavulana2066 huku ikikabiliwa  na upungufu wa vyumba  vyumba 70  kwa sasa vilivyopo 11 mapungufu ya vyumba vya madarasa ni 59.
Kadongo alisema kutokana na upungufu huo serikali imetoa Tsh milion 66.6  kutoka mfuko wa P4R kati ya fedha hizo Sh milioni 60 kwa ajili ya vyumba vitatu vya madarasa Sh 6.6 milioni  kwa ajili ya matundu sita ya choo cha wanafunzi kwa sasa matundu ya choo yanayo tumika 16 wavurana 8 na wasichana 8.
 
Kadogo aliomba serikali kuendelea kuiangalia shule hiyo kutokana na kukabiliwa na changamoto nyingine ya upungufu wa walimu mahitaji walimu 70 waliopo 25 na kwamba upungufu wa madarasa.
Afisa Elimu Shule za Msingi Wilaya ya Bukombe Shadurack Kabanga alisema fedha hiyo imetoka serikali kuu nakwamba iwapo madarasa hayo yakikamilikaa ifikapo mwenzi Juni yatasaidia kuondoa changamoto ya wanafunzi kubanana darasani.
Kabanga alisema Wilaya ina shule za msingi 78 za serikali na zinakabiliwa na changamoto mbali mbali ikiwemo upungufu wa nyumba za walimu na madarasa ingawa wananchi wanaendelea kujenga na serikali inaunga mkono nguvu za wananchi hao.

Comments