JPM AHIMIZA WANANCHI KUTUNZA MIUNDOMBINU YA MABARABARA




Wananchi Mkoani Geita wahimizwa kulinda na kutunza miundombinu ya mabarabara kwa manufaa ya watanzania wote.
Aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa barabara ililo jengwa kwa kiwango cha lami  kutoka Uyovu kwenda Bwanga yenye urefu wa kilomita 45 liligalimu Sh47bilioni mkandarasi amesha lipwa sh20 bilioni nakuongeza kuwa atakapo fika ikulu atasaini malipo ya sh27bilioni zilizo baki kwa ajili ya mkandarasi huyo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli aliwapongeza Wizara ya Ujenzi kwa kushirikiana vizuri  na mkandarasi (SINO HYDRO) nakuongeza kuwa Tanzania anayoiongoza yeye watumishi wa umma wahakikishe wanawasikiliza wanyonge.
Magufuli aliwakumbusha Wakurugenzi Watendaji wa halmashauri, Wakuu wa Wilaya na Mikoa nchini kusimamia agizo lake la kutetea wakulima kwa kutowatoza ushuru wanapo safirisha mazao yao chini ya tani moja huku akisisitiza wasitozwe ushuru wa aina yeyote kwani sheria imepitishwa na bunge.
“katika uongozi wangu sitapenda watanzania wa maisha ya chini wanyanyaswe, nitapenda watanzania waishi kwa amani nitapenda watanzania washirikiane bila kujali itikadi za dini,ukabila wala vyama vyao watanzania tudumishe umoja mshikamano na uzalendo na kila mmoja ajipange kuleta maendeleo ya kuinua uchumi wa nchi yetu”.alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli aliwahimiza viongozi mbali mbali wa madhehebu ya dini,wazee,viongozi wa kimila,vijana na kinamama kuombea na kuilinda amani ya Tanzania ikiwa taifa limekaa kwa amani zaidi ya miaka 50 na kuwa mfano kwa mataifa mengine
Aliwaomba wakulima na wafungaji kuwa wavumilivu wakati serikali inajipanga kukata sehemu ya maeneo ya mapori ya hifadhi za serikali  kuwa ardhi ya makazi na eneo la kufanyia shughuli mbalimbali za kibinadamu huku akiwaahadi wakulima na wafugaji kuwa atalisimamia na kuhakikisha wanafaidika na jasho lao lengo ni kuimarisha maisha ya watanzania ki uchumi.
Aliwapongeza watumishi wa Tanroads akiwemo Mhandisi Mfugale kwa kufanya kazi nzuri pamoja na wenyeviti wa bodi na kuwasihi waendelee kusimamia barabara, “nawakumbuka sana natamani kurudi kwenye Wizara ya Ujenzi kwasababu ni Wizara nimeka katika maisha yangu miaka 17  watumikieni watanzania”.Alisema Rais Magufuli.
Rais Magufuli aliwaomba wananchi kuto badilika badilika katika uchanguzi kwani mwaka 2015 walichaguwa Mbunge mzuri na kwamba amekuwa mwenyekiti wa kamati ya madini amefanya vizuri akaenda kuchunguza madini ya tanzanite amefanya vizuri na hatimae kumuona kumteuwa kuwa Naibu Waziri wa Madini na anafanyakazi nzuri mpeni ushirikiano.
Awali Naibu Waziri wa Wizara ya Ujenzi Elias Kwandikwa akimkalibisha Rais Magufuli kuongea na mamia ya wananchi waliohudhulia kwenye viwaja vya eneo la kanisa  katoriki Kata ya Uyovu Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita waliotoka vijiji mbali mbali vinazounda Wilaya ya Bukombe kwa ajili ya kumsikiliza.
 Kwandikwa alisema barabara ya Uyovu kwenda Bwanga yenye urefu wa kilomita 45 inaunganisha barabara ya Busagara,Geita, na Bihalamulo, yenye urefu wa kilomita 220.
Alisema pia barabara ya Uyovu Bwanga inaunganisha barabara kuu ya kutoka Isaka Ushirombo Lusumo yenye kilomita 374 barabara hii imeunganisha wananchi wa Mkoa wa Geita Shinyanga Kagera Kigoma na nchi jirani za Burundi, Rwanda na nchi ya kidemokrasia ya watu wa Kongo (DRC) na Uganda.
Kwandikwa alibainisha malengo ya utekelezaji wa mradi huu ni kuhakikisha wananchi wa maeneo hayo kuazia wakulima na wavuvi wafanya biashara wanakuwa na barabara zinazo pitika munda wote, kukamilika kwa mradi huu kumefungua furusa ya kusafirisha watu na bidhaa.
Kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Bukombe Mbunge wa Jimbo la Bukombe pia Naibu Waziri wa Madini Doto Mashaka Biteko alimshukuru Rais Magufuli kwa kufika tena kuonana na wananchi wa Wilaya ya Bukombe wananchi waliokuwa wamemkumbuka na ahaidi zake alizozitoa kwenye kampeni vitendo vyake vimedhibitika kwa vitendo.
“kunamiradi ilikuwa haipo lakini umetumwagia fedha ikiwemo kumaliza changamoto ya shule ya msingi Ibamba uliitatua kero hiyo ,pia umetoa Sh500 milioni kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa chumba cha upasuaji kituo cha afya Ushirombo na kituo cha afya Uyovu Sh 400 milioni kwa ajili ya ujenzi wa wondi ya mama na mtoto pia  magari mawili ya kubeba wagonjwa kituo cha afya Uyovu na kituo cha afya Ushirombo Rais anajuwa shida za watanzania wananchi wanasema ni mwambie zile kilomita tano za lami anajuwa barabara ya ushirombo katoro kuwa wananchi wanaomba liwekewe lami anajua maji kutoka ziwa viktoria amesha tenga Sh1,7 Bilioni anajuwa munahitaji maji kutoka ziwa viktoria mimi siwezi kusema na wanaotaka nimwambie Rais kilakitu anajuwa”alisema Biteko.
Biteko aliwaomba wananchi kuendelea kumuunga mkono na kumuombea Rais Magufuli aendele kutetea haki za wa watanzania wa maisha ya chini na kuleta mabadiliko ya taifa hasa katika kupandisha uchumi wa taifa.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Robert Luhumbi kwa niaba ya wananchi wa Mkoa wa Geita alimshukuru sana Rais Magufuli kuja kufungua barabara hiyo ambayo inachochea maendeleo ya kiuchumi na  fursa za kiuchumi na kijamii kwa kiasi kikubwa ikiwemo na ukuwaji wa sekta za kibiashara sekta ya kilimo na kurahisisha usafirishaji watu na mazao barabara hiyo itachochea ukuaji wa sekta ya utalii na kuongeza pato la Mkoa na taifa kwa ujumla.
Mkazi wa Kata ya Uyovu Letisia Mourice alisema serikali imefanya vizuri kutengeneza barabara hiyo kwani kumewaondolea changamoto ya kusafiri kwenda Bwanga walikuwa wana tumia masaa mawili barabara lilikuwa bovu lakini kwa sasa watasafiri kwa magari watatumia dakika 40 hali ambayo itawafanya kuwa na mzunguko mkubwa wa kiuchumi na kurahisisha ndugu na jamaa kufika kwenye huduma za afya mapema.
 

Comments