Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Bukombe wameadhimisha miaka 41 ya CCM kwa kuchota baraka

 Jiko la kisasa kwa ajili ya kuwapikia wanafunzi wa kitengo cha elimu maalum kilichopo Shule ya msingi Ushirombo.
Hawa ni baadhi tu ya wanafunzi wa kitengo cha elimu maalum kilichopo Shule ya msingi Ushirombo.
  Vyumba vya Madarasa  kwa ajili ya wanafunzi wa kitengo cha elimu maalum
 Katibu wa Wazazi Mkoa wa Geita Joseph Mwita akizungumza na wanaccm katika maadhimisho yaliyofanywa na Jumuiya ya Wazazi Ccm(W)Bukombe katika shule ya Msingi Ushirombo kitengo cha elimu maalum.
 Meza Kuu
 Wajumbe.
 Mmoja ya Wajumbe akizungumza katika hafla hiyo.
  Katibu wa Wazazi Mkoa wa Geita Joseph Mwita akiendesha zoezi la upandaji miti katika shule hiyo


















Jumuiya ya Wazazi CCM Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita wamefanya maadhimisho ya miaka 41 ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwa kuwatembelea wanafunzi wa shule ya msingi Ushirombo kitengo cha elimu maalum na kufanya usafi,changizo la kiasi cha shilingi elfu themanini na kushiriki nao kwenye chakula cha mchana shuleni hapo.
Katika maadhimisho hayo Katibu wa wazazi Mkoa wa Geita Joseph Mwita amewashukuru wanachama kwa uamuzi wao wa busara  kwenda kuwaona watoto hao huku akisisitiza zoezi hilo kutokukomea leo.
Pia waalimu wa shule hiyo walibainisha  changamoto zao ikiwa ni ukosefu wa usafiri kwa watoto kwani asilimia kubwa ya watoto hao hawajiwezi kwenda na kutoka shuleni peke yao,upungufu wa miundo mbinu ya madarasa kulingana na ongezeko la idadi ya wanafunzi hao kwa sasa pamoja na vifaa vya michezo.
Aidha Katibu wa wazazi Mkoa wa Geita Joseph Mwita amewaomba wanachama wa CCM na wananchi kwa ujumla wajitahidi kuwahudumia watoto hao sambamba na kuwafichua kwa pamoja baadhi ya watoto wenye ulemavu waliofichwa na wazazi wao au walezi majumbani bila kupata elimu ili nao waweze kujipatia elimu.


Comments