UMOJA WA VIKUNDI KUMI NA SITA KUTOKA UYOVU KUWEZESHWA NA MHE. DOTO BITEKO

Meza Kuu
Mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake  Wilaya ya Bukombe Leticia Mourice akisoma risala
Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Mkoa wa Geita Jazaa Komba akizungumza katika hafla hiyo.
Mhe. Diwani wa Kata ya Igulwa akila keki
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na umoja wa vikundi kumi na sita vya wamama Kata ya Uyovu.


Wamama wanaowekeza pesa zao katika jukwaa la wanawake Wilayani Bukombe  wametakiwa kuzitumia fedha wanazozipokea kutoka kundi hilo ili kujiimarisha kimaisha.
Akizungumza katika sherehe iliyojumisha vikundi kumi na sita vya Kata ya Uyovu walipokutana kwa ajili ya kugawana faida,kufahamiana na kubadilishana uzoefu.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko wakati akijibu changamoto za wamama hao alianza kwa kuwapa taslimu milioni moja  kwa ajili ya kuinuia mfuko wa umoja wa wanawake hao sambamba na kuwasisitiza kutafuta eneo la kujenga ofisi kwa ajili  ya kuongeza thamani ya umoja huo na kupata sehemu ya kudumu kwa ajili ya ujasiliamali hali  iwatakayowapa jumuiya zingine kuona mfano ndani ya Kata ya Uyovu na Wilaya nzima ili kupunguza wimbi la wasio na ajira huku wakimuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mhe Dkt John Pombe Magufuli katika Tanzani ya Viwanda

Comments