MKUU WA MKOA WA GEITA AAGIZA MSAKO WA WANAFUNZI WALIOSHINDWA KURIPOTI SHULE




Wazazi na walezi ambao hawajawapeleka wanafunzi waliofaulu kuanza kidato cha kwanza kuanza kusakwa wakiwemo wanafunzi wenyewe.


Agizo hilo la kuazishwa msako lilitolewa na Mkuu wa Mkoa wa Geita,Mhandisi Robert Luhumbi wakati akipokea taarifa ya uadikishaji wa wanafunzi kitado cha kwanza mwaka 2018 iliotolewa na Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Bukombe wakati wa ziara yake ya kikazi Wilayani Bukombe.

Luhumbi aliagiza msako huo kuanzia Januari 22 kuwasaka wanafunzi na kuwakamata wazazi na walezi ambao hawaja wapeleka wanafunzi kuadikishwa na kuhakikisha  wanafunzi wote wanapelekwa shule.

Awali Afisa Elimu shule za Sekondari Wilaya Philibert Nyangahondi alisema Wilaya ina shule 14  za sekondari za serikali ambapo zilitakiwa kupokea jumla ya wanafunzi 3985.


Nyangahondi alisema wanafunzi wa kitado cha kwanza wanaotakiwa kuripoti ni 3985  hadi kufika Ijumaa ya januari 19 mwaka huu walikuwa wamelipoti wanafunzi 2829 bado wanafunzi 1156 ambao haijulikani walipo.

Mkuu wa Mkoa Mhandisi Luhumbi aliagiza kamati za ulinzi na usalama  Wilaya zote za Mkoa wa Geita kuwashukia viongozi ngazi ya Kijiji ili kuhakikisha wanafunzi wanaripoti shuleni na waliofikia umri wa kuadikishwa darasa la kwanza wanapelekwa shule.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga alimhakikishia Mkuu wa Mkoa atatekeleza agizo hilo  mapema.
 
Maganga aliwaomba wazazi na walezi kupeleka wanafunzi mashuleni kabla ya kukamatwa na kufikishwa kwenye vyombo vya dola.

Comments