MKUU WA MKOA GEITA APIGA MARUFUKU BODI ZA SHULE KUPITISHA MICHANGO KWA WAZAZI




Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Luhumbi amepiga marufuku bodi na kamati za maendeleo ya shule kuratibu michango kwa wazazi na walezi mashuleni.
Luhumbi aliyasema hayo baada ya kupokea taarifa ya fedha Sh milioni 60  toka  P4R ambazo zimeelekezwa na serikali kujenga vyumba vya madarasa sita  katika shule ya sekondari Ushirombo huku bodi ya shule hiyo ilikuwa inakusanya tofari tatu toka kwa wazazi kwa ajili ya ujezi huo.

Luhumbi alibaini kuwa ripoti aliyoipokea ilikuwa na nia nzuri lakini imefanyika katika mazingira mabaya kunamahitaji ya vyumba vya madarasa  lakini bodi ya shule hiyo iliwataka wazazi na walezi kukubaliana kuazisha ujenzi  kwa michango ya tofari tatu hali ambayo inaathiri taratibu zinazotaka kutowaumiza wazazi kwani miongoni mwao kunawananchi wanaishi mazingira magumu wakiwemo  wanufaika wa mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF.

 Alisema serikali haitaki kuweka michango kwa mzazi yeyote badala yake michango ya kuchangia maendelo ya ujenzi wa shule zahanati wahusishwe wananchi wote na sio wazazi  shuleni, wanafunzi wasirudishwe nyumbani kwa tatizo la michango alisema Mkuu wa Mkoa Luhumbi.
Luhumbi alisema kutokana na hii taarifa kunakundi kubwa liliachwa kushirikishwa wakiwemo wadau wa Elimu na wafanyabiashara huku akiwasihi madiwani kufanya mikutano ya hadhara kuhamasisha michango ya hiyali kwenye miradi ya maendeleo.
Akiwa shuleni hapo Mkuu wa Mkoa Luhumbi, wananchi walimunga mkono na kufanya harambee fupi na kufanikisha kukusanya mifuko 84 ya saruji fedha Sh 110,000 tofari 30 za sementi na tripu za mchanga 2 kutoka kwa wananchi.
Luhumbi aliwata wahusika wa mradi wa ujenzi wa madara sita na ofisi mbili za walimu hadi kukamilia zisitumie Sh 60 milioni nakuwashauri  kutoa tenda za ujenzi kuanzia kuchimba msingi na kazi ndogo ndogo washirikishwe wananchi ili kuokoa gharama zisizo kuwa za lazima ili kuokowa fedha hizo ili zitakapo baki zifanye kazi nyingine ya maendelo .
Awali mkuu wa shule ya Ushirombo Sekondari Juma Luguhwa alisema  kikao cha desema 14 cha wazazi kilichotanguliwa na kikao cha walimu cha Desemba 7 kikifatiwa na kikao  cha Bodi cha Desemba 15 wazazi na walezi walikubaliana kuazisha ujenzi wa vyumba vya madarasa viwili  kila mwanafunzi anaesoma hapo mzazi alete tofari tatu.]
Luguhwa alisema walitarajia kukusanya tofari 4,545 hadi Rais Dk John Magufuli anazuia michango walikuwa wamekusanya tofari 1,038  na kwamba Desemba 29 mwaka 2017 shule iliigiziwa fedha Sh 60 milioni kutoka mfuko wa P4R kikao kilihudhuliwa na wazazi 100 lakini wako zaidi ya 200.
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Bukombe Daniel Machongo amempongeza Mkuu wa Mkoa kufika kuwaunganisha viongozi na wananchi na kuwapa Elimu ya kuto chagishwa shuleni badala yake wachangie kupitia mikutano ya serikali itakayofanywa na madiwani kuhamasisha michango ya hiyali ya maendeleo kwa wananchi ili kukamilisha miradi.

Comments