RUNZEWE ACADEMY FC KUJINYAKULIA TENA USHINDI KWENYE LIGI YA DOTO CUP 2017


Vikosi vya Basketball vikiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Vikosi vya Mbio za baiskeli vikiwa uwanjani katika ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Vikosi vya Volleyball vikiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Vijana wa Karate wakiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Vijana shupavu wakionyesha uwezo wao uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Vikosi mbalimbali  vikiwa pamoja na mashabiki tayari kwa maandamano ya pamoja na kupokea ujumbe wa Bonanza la Doto Cup 2017
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akitoa ujumbe wa  Bonanza la Fainali ya  Doto Cup 2017 mara baada ya kuwasili mgeni rasmi.
Vikosi vya wakimbia kwenye magunia wamama vikiwa uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Fainali Doto Cup 2017
Mshindi wa kukimbiza kuku upande wa wanaume
Mshindi wa kukimbiza kuku upande wa wanawake
Mashabiki na wanachama wa Simba na Yanga wanawake wakipimana nguvu  uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Mashabiki na wanachama wa Simba na Yanga wanaume wakipimana nguvu  uwanjani kwenye ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Said Kiganja akikagua wachezaji wa Netball ushiriki wa Bonanza la Doto Cup 2017
Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Said Kiganja,Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb),Mwenyekiti wa CCM(W) Daniel Machongo na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe wakiwa na wachezaji wa Timu ya Runzewe Academy Fc katika Picha ya Pamoja kabla ya mchezo kuanza wa Fainali ili kumpata mshindi  wa  Ligi ya Doto Cup 2017.

Katibu Mkuu wa Baraza la Michezo Said Kiganja,Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb),Mwenyekiti wa CCM(W) Daniel Machongo na Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga wakiwa na wachezaji wa Timu ya Chui Fc kutoka Bugerenga katika Picha ya Pamoja kabla ya mchezo kuanza wa Fainali ili kumpata mshindi  wa  Ligi ya Doto Cup 2017.

Wana-Bukombe wakishuhudia uhondo wa michezo mbalimbali katika Bonaza la Fainali hiyo ya Doto Cup 2017.


Timu ya Runzewe Academy Fc imetwaa ubingwa wa lingi ya Doto Cup 2017  kwa kuichapa timu ya Chui fc iliyoko Bugelenga  gori 8 -7.


Wafungaji wa magori ya Runzewe Academy John Ngasa dakika ya 18 kipindi cha kwanza na Leonard Figo dakika ya 80 kipindi cha pili huku magori 6 yakifungwa kwa mikwaju huku gori la ushindi lilifungwa na Rashid Sanga kwa penaliti.


Magori ya Chui fc yalifungwa na Jonas Jemes dakika ya 50 na Musa Jemes dakika ya 66 na wakati wa kucheza matuta kutokana na dakika 90 kuisha bila kupatikana mshindi wa chezaji wa Chui fc walifunga magori kwa penaliti 5 na kuchukuwa nafasi ya pili.


Mbunge wa jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko mudhamini wa lingi hiyo alisema lengo la kuandaa mashindano  nikuwatambua na kuwainua vijana kimichezo.

Mhe. Biteko  wakati akimuomba Katibu Mtendaji Mkuu wa Baraza la Michezo Tanzania kuvionea kipaumbele vipaji vya vijana wanao ishi kwa kucheza ndodo ili wakapatiwa na fasi kwenye timu kubwa za taifa.


Katibu msaidizi wa chama cha mpira wa miguu wilaya ya Bukombe (BUFA) Erasto Banunu alisema ligi hiyo iliaza Julai 15 mwaka huu na kushirikisha vilabu 128 michezo waliyo cheza hadi siku ya fainali michezo 120.


Alisema wilaya ya Bukombe inavijana wenye vipaji kwenye Soka lakini hawana wakuwaendeleza hivyo kupitia Baraza la Michezo na TFF ilete walimu wakufundisha na kutambua vipaji kwa vijana.


Katibu mtendaji wa Baraza la Michezo Tanzania Said Kiganja ambae alikuwa mgeni rasmi kwenye fainali ya Doto Cup 2017 kabla hajakabizi zawadi alimpongeza Mhe Mbunge kwa kuisaidia serikali kujibu utekelezaji wa ilani ya chama cha mapinduzi ibara ya 161.


Kiganja alikubali ombi la Mbunge na kumtaka kufanya mambo ya fuatayo mwaka 2018 atakapo kuwa anafanya madalizi ya ligi ashirikishe ofisi yake na wachezaji wa lingi ya mwaka 2018 wawe wenye umri 15 hadi 17 ili baada ya mashindano hayo baadhi ya vijana watachukuliwa kujiunga na timu ya watoto ya taifa.


Mshindi wa kwanza Runzewe Academy Fc ilikabiziwa kombe la ushindi wa Ligi ya Doto Cup 2017 yenye thamani ya sh 300,000 na kitita cha fedha Sh 500,000 seti tatu za jenzi mipira mitatu cheti cha ushiriki.


Timu ya Chui fc ya Bugelenga washindi wa pili walibeba sh 300,000 seti za jenzi mbili mipilia miwili na cheti cha kushiriki huku mshindi wa tatu Kurugenzi fc ya Katente walijinyakulia sh 200,000 seti ya jezi moja mpira moja na cheti cha ushiriki.

Comments