
"Alifanyiwa
vipimo siku mbili zilizopita na atakuwa nje kwa muda fulani - sifahamu;
wiki mbili au wiki moja zaidi? Lakini hatakuwepo. Nafikiri hatacheza
Stoke. Kwetu, Alexis Sanchez ni pigo" alisema Wenger.
Alipoulizwa
kama Sanchez, ambaye amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake atasaini
mkataba mpya, Wenger alisema: "Wakati wote inawezekana. Mchezaji
anapokuwa katika mwaka wa mwisho (wa mkataba wake) wakati wote
tutajaribu kumuongezea," alisema. "Hakuna sababu ya kutofanya hivyo.
hatujafika huko bado,"alisema.
Comments
Post a Comment