Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akifanya shunguli ya kuranda mbao kwenye moja ya ofisi kijiwe maarufu maeneo ya Msonga alipowasili kwa ajili ya kuzungumza na mafundi hao
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mhe. Safari Nikasi Mayala akizungumza na mafundi hao
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na mafundi sermala hao maeneo ya Msonga Kaya ya Runzewe Mashariki
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisindikizwa na baadhi ya mafundi baada ya mazungumzo
Jamii
hasa vijana wemeombwa kuacha kufanya siasa za tangu januari hadi desemba bila
tija na badala yake wajiunge katika vikundi kwa pamoja bila kujali itikadi,dini
wala ukabira wao ili waweze kusaidiwa na serikali kwa haraka zaidi hatimaye kujipatia kipato kihalali .
Hayo
yalisemwa leo na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko alipofanya
ziara kwenye Kata ya Runzewe Mashariki na kuzungumza na baadhi ya vijana wanao
jihusisha na ufundi seremala na
kusikiliza changamoto zao.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mhe. Safari Nikasi Mayala alisema, haikubaliki vijana na jamii kutumika katika mambo ya ovyo badala ya kujenga taifa, hali ambayo inayowasababishia vijana wengi kutokufanya kazi na kuranda mitaani kwa kisingizio cha kuisubiri serikali iwaletea maendeleo bila wao kushiriki chochote.
Kwa upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mhe. Safari Nikasi Mayala alisema, haikubaliki vijana na jamii kutumika katika mambo ya ovyo badala ya kujenga taifa, hali ambayo inayowasababishia vijana wengi kutokufanya kazi na kuranda mitaani kwa kisingizio cha kuisubiri serikali iwaletea maendeleo bila wao kushiriki chochote.
Nae
Mwenyekiti wa Mafundi seremala hao Alex Gervas amshukuru sana Mhe. Doto Mashaka
Biteko(Mb) kwa ujio wake na kumweleza changamoto na uhitaji wa mafundi seremala
hao ikiwa ni pamoja na kupanda kwa ushuru wa vitanda kutoka elfu kumi na mbili ya awali hadi laki
moja elfu mbili kwa sasa hali inayowasababishia kutofuanya uzalishaji mkubwa
kutokana na changamoto hiyo.
Pia
walimuomba Mbunge Doto kuwasaidia ili waweze kutambulika kisheria sambamba na
kupata vyeti vya VETA.
Comments
Post a Comment