TIMU YA SILAMILA YA IBUKA KIDEDEA KATIKA LIGI YA DOTO CUP 2017 NGAZI YA KATA



 Timu zikisikiliza maelekezo kabla ya mchezo kuanza yaliyokuwa yakitolewa na Katibu wa Chama Cha Mpira Wilaya ya Bukombe (BUFA) bw. Bosco Mwidadi
  Timu ya Butinzya Fc wakipeana mikono na meza kuu baada ya kumaliza mchezo
  Kiongozi wa Timu ya Butinzya Fc akipokea zawadi ya mpira mpya kabisa kutoka kwa Mhe. Diwani wa Kata ya Butinzya Mhe. Amos Shimo  ikiwa ni zawadi ya mshindi wa pili katika fainali hiyo.
   Timu ya Silamila Fc wakipeana mikono na meza kuu baada ya kumaliza mchezo


  Kiongozi wa Timu ya Silamila Fc akipokea zawadi ya Jezi  mpya kabisa kutoka kwa Mhe. Diwani wa Kata ya Butinzya Mhe. Amos Shimo  ikiwa ni zawadi ya mshindi wa kwanza  katika fainali ya Doto Cup 2017 ngazi ya Kata-Butinzya.
 Kama kawaida yetu mashabiki baada ya Ushindi na kujionea zawadi mubashara.

 Timu ya Silamila Fc iliyopo  Kata ya Butinzya  Wilayani Bukombe Mkoani Geita jana imejinyakulia  zawadi ya Jezi mpya ikiwa ni zawadi kwa mshindi huyo kwa ngazi ya Kata katika Ligi ya Doto Cup 2017  baada ya kuichapa gori 3-0 Timu ya Butinzya  Fc katika hatua ya fainali  iliyohitimishwa hapo jana katika uwanja wa Shule ya Sekondari Butinzya.

Mechi hiyo iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki katika uwanja wa Shule ya Sekondari Butinzya  Timu ya Silamila  ilichapa gori 3 Timu ya Butinzya Fc kupitia kwa Nzala Nangi,Benjami Dominiko na kiungo mshambuliaji Roja Charz.

Hadi dakika tisini ya mchezo huo Timu ya Butinzya fc haikupata hata gori la kufutia chozi.

Wakati akifungua mchezo huo  Katibu wa Chama Cha Mpira Wilaya ya Bukombe (BUFA) bw. Bosco Mwidadi ilisema



Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo,  Diwani wa Kata ya Butinzya Mhe. Amos Shimo alizishukuru timu zote kwa ushiriki wao na kuelezea alichojifunza katika Ligi hiyo ya Doto Cup 2017

Comments