Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisaini kwenye kitabu cha wageni baada ya kuwasili katika Kituo cha Polisi Runzewe.
Mkuu wa Kituo cha Polisi Runzewe hicho Insp. Richard Godbless Mkesi akimweleza Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisalimiana na baadhi ya wananchi waliokuwa maeneo ya kituo hicho cha polisi Runzewe.
Mkuu wa Kituo cha Polisi Runzewe hicho Insp. Richard Godbless Mkesi akimweleza Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.
Picha ya Kituo cha Polisi Runzewe.
Haya ni magari ya Kituo cha Polisi Runzewe
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka
Biteko akisalimiana na baadhi ya askari polisi wa Kituo cha Polisi Runzewe.Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisalimiana na baadhi ya wananchi waliokuwa maeneo ya kituo hicho cha polisi Runzewe.
Polisi wa Kituo cha
Runzewe Wilaya ya Bukombe Mkoani
Geita wamemuomba Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko
kuwatatulia changamoto ya usafiri kwenye Kituo hicho cha Polisi Runzewe.
Wakati akizungumza Mkuu wa Kitu hicho Insp. Richard Godbless
Mkesi amesema hali ya usalama kwa maeneo hayo iko shwari na kumbainishia
changamoto ya ukosefu wa usafiri kituoni hapo kutokana na uchakavu wa magari na
kukosa matengenezo ya magari hayo kunawasababishia hali ya kufanya shuguli zao za kiusalama kwa
kuazimaazima usafiri.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka
Biteko aliwashukuru kwa kazi nzuri ya kuimarisha ulinzi na usalama wa maeneo
hayo na kuwaomba polisi hao kuzidi kuwaelimisha wananchi juu ya kutii sheria
bila shurti hasa kwenye vyombo vya moto.
Pia aliahidi kushirikiana na polisi hao pamoja na wananchi wa
maeneo hayo na Wilaya nzima kwa ujumla katika kuhakikisha watumiao vyombo vya
moto hasa bodaboda wanapatiwa mafunzo ya usalama barabarani ili kupunguza ajali
na vifo visivyokuwa vya lazima na hatimae kupoteza nguvu kazi ya taifa.
Comments
Post a Comment