HOFU YATANDA HOSPITALI YA MAJERUHI KIBITI


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Rufiji, Onesmo Lyanga.
KIBITI: Hofu kubwa imetanda kwa wagonjwa na wauguzi wa Hos­pitali ya Mchukwi iliyopo Kijiji cha Songa, Kibiti mkoani Pwani, am­bayo majeruhi wanaotoka­na na uhalifu unaoendelea katika maeneo ya Ikwiriri, Kibiti na Rufiji wanatibiwa.Kwa mujibu wa wauguzi hao, walioomba hifadhi ya majina yao kwa kuhofia usalama wao, kitendo cha kuwaweka majeruhi hao hospitalini hapo ni hatari kwao na hata wahudumu wenyewe, endapo wauaji hao wataamua kwenda ku­wamalizia baada ya kuwa­kosa huko majumbani.Hawa watu wanafanya mauaji kwa malengo am­bayo hayafahamiki, sasa tunahofia ipo siku watataka kuja kuwamalizia hapa­hapa, sijui itakuwaje maana hata sisi sasa tuna hofu kubwa sana, hatuna ulinzi kwa hiyo wakija watatuoko­ta tu kama kuku,” alisema muuguzi huyo.
Licha ya kilio cha us­alama wao, pia wauguzi hao walisema kitu kingine kinachowapa tabu ni kuko­sekana kwa mawasiliano ya simu, kwani eneo hilo halina ‘network’ kwa muda mwingi.
Akizungumzia hilo, mmoja wa wauguzi hao alisema licha ya eneo hilo kuwa na wakazi wengi wa­naohitaji huduma ya ma­wasilino ya simu, lakini hali ni ngumu sana.
“Sasa kwa mfano hata kama wakija hapa hao wa­halifu, itachukua muda mrefu sana kupata msaada kwa sababu hatuwezi ku­piga simu kwa wakati.
“Inafikia wakati tunataka kumpa mgonjwa rufaa ya kuelekea Hospitali ya Taifa ya Muhimbili au hospitali nyingine, lakini tunashindwa kufanya mawasiliano na huko tunakotaka kumpeleka.
“Wakati mwingine tu­nahitaji kutuma nyaraka mbalimbali za kikazi kupitia mitandao au kwa kuwasil­iana na madaktari wa sehe­mu nyingine, lakini hilo nalo linakuwa gumu kwa ajili ya kusaidiana mawazo lakini hilo nalo linakwama.
“Tunaziomba kampuni za simu zituletee huduma huku jamani, maana hata ukiacha­na na hii hospitali huku kuna watu wengi wanaohitaji hu­duma ya mtandao,” alisema muuguzi huyo.
Vitendo vya mauaji ya raia na viongozi wa vijiji na seri­kali za mitaa vinaendelea ku­tikisa katika Wilaya za Kibiti, Rufiji na Mkuranga mkoani Pwani na hivyo kuwa tishio kubwa kwa wananchi.

Comments