DEREVA wa basi la
abiria la AM Coach, Andrea Jafari (42) amefikishwa katika mahakama ya wilaya ya
Mlele mkoani Katavi jana kwa kosa kumuua Twiga anayekadiriwa kuwa na thamani ya
zaidi ya Sh Milioni 33 baada ya kumgonga kwa uzembe.
Jafari ambaye ni
mkazi wa Tabora amerudishwa rumande hadi Julai 14 kesi yake itakapotajwa tena
baada ya kushindwa kukidhi vigezo vya dhamana ambavyo vilimtaka aache
mahakamani hapo nusu ya thamani ya Twiga aliyemuua ambayo ni zaidi ya Sh
Milioni 16.5 na hati ya mali isiyohamishika ambayo imethibitishwa na mtathimini
yenye thamani ya zaidi ya Sh Milioni 16.5.
Comments
Post a Comment