ACACIA Yakubali Kulipa mirabaha iliyowekwa katika sheria mpya ya madini

Kufuatia mabadiliko yaliyofanywa na Bunge katika sheria za usimamizi wa rasilimali nchini, ongezeko la mrabaha unaotarajiwa kulipwa serikali uliongezeka kutoka katika asilimia 4 iliyokuwa katika sheria za zamani.

Katika kuonyesha kukubaliana na mabadiliko hayo, Kampuni ya uchimbaji madini nchini ya Acacia imekubali kuilipa serikali mrabaha wa asilimia 6 unaoendana na sheria mpya zilizoanza kutumika mwezi huu mwanzoni baada ya kusainiwa na Rais Julai 5.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na kampuni hiyo leo inaeleza kuwa, ili kuepuka mkanganyiko au mvurugano zaidi kwenye kazi zao katika siku za usoni, watatimiza matakwa yanayohitajika katika ongezeko la mrabaha wa katika madini ya dhahabu, fedha na shaba la asilimia 6.

Comments