Mbunge
wa Kigoma Mjini kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo, Zitto Kabwe
amemsifu Rais Dkt Magufuli kwa jitihada zake za kupambana na rushwa
ambapo amesema kwa muda wote, leo ameona kuwa vita ya ufisadi ina maana
kubwa.
Zitto
ameyasema hayo jana kupitia ukurasa wake wa Twitter ambao aliandika
jumbe kadhaa kupongeza jitihada hizo za Rais Magufuli ambapo katika moja
ya jumbe zake alisema kuwa, kukamatwa kwa watuhumiwa hao wa sakata la
Tegeta Escrow ni moja ya hatua kubwa sana za Rais Magufuli dhidi ya
rushwa.
Zitto
alisema kuwa licha ya kuwa amekuwa akimpinga Rais Magufuli katika mambo
mbalimbali na ataendelea kumpinga, lakini katika hili la kukamatwa kwa
James Rugemarila na Harbinder Sethi anamuunga mkono na kumpongeza sana.
Comments
Post a Comment