BULEMBO AMALIZA MIZIZI YA CHADEMA - CHATO, MKURUGENZI WA ULINZI NA USALAMA WA CHADEMA KUHAMIA CCM.

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wanaCCM pamoja na wakazi wa Buzilayombo Wilayani Chato  wakati akielekea Wilayani humo kwa ajili ya kufanya kikao na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Chato, Wajumbe wa Mabaraza ya Jumuiya za CCM, Madiwani, Mabalozi na Watendaji wa Serikali, katika Ofisi ya CCM ya Wilaya hiyo Mkoani Geita, leo Juni 9, 2017.
Wajumbe wakishangilia Ukumbini wakati Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Bulembo alipokuwa akiwasili ukumbini humo kwa ajili ya kikao.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Bulembo akielekea eneo la kukaa tayari kwa kuanza  kikao hicho, leo
  Kikundi cha CCM, wakitumbuiza  kabla ya  kikao hicho kuanza , leo
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Bulembo akisaini kitabu cha wageni baada ya kuwasili ukumbini. Kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Geita Kasheku Msukuma na kulia ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Chato Ibrahim Bagula
Ofisa kutoka Makao Makuu ya Jumuia ya Wazazi Tanzania Omari Kalolo akiimba nyimbo za hamasa kabla ya kujitambulisha kwenye mkutano huo
Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Chato Ibrahimu Bagula akizungumza kwenye kikao hicho
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi Mkoa wa Geita na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akitoa salamu na kuhamasisha wanaCCM wa Wilaya ya Chato na Mkoa wa Geita kwa Ujumla kuzidisha umoja ili kukipa nguvu zaidi Chama Cha Mapinduzi CCM.  
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM wa Mkoa wa Geita Sukuma Kasheku akizungumza katika kikao hicho

Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akizungumza na wajumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Chato, Wajumbe wa Mabaraza ya Jumuiya za CCM, Madiwani, Mabalozi na Watendaji wa Serikali, katika Ofisi ya CCM ya Wilaya hiyo ya Chato.

WanaCCM wakishangilia kwa furaha




Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Alhaj Abdallah Bulembo akiagana na wajumbe baada ya kikao hicho.




Comments