Katibu mpya wa CCM Mkoa wa Geita amefanya ziara ya kwanza katika Wilaya ya Bukombe










Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Geita Comrade Adamu Paul Ndalawa amefanya ziara yake ya kwanza Wilayani Bukombe na kuzungumza na baadhi ya viongozi, watendaji na wanachama wa Chama cha Mapindizi (CCM) wa Wilaya ya Bukombe.

Katika ziara hiyo Bwn. Ndalawa amewaeleza kuwa ni wakati wa wanaCCM hao kubainisha nini vipaumbele vyao katika kusukuma maendeleo ya Wilaya ya Bukombe. 
   
Moja ya vibaumbele vya wanachama hao kwa Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Geita Comrade Adamu Paul Ndalawa  ni kuendelea kujenga umoja wa wanachama na jumuiya zake kwa vitendo na kumhakikishia kupata Hati miliki ya eneo la ofisi hiyo ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Bukombe bila kuchelewa.
 
 Aidha kwa upande wake Katibu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Mkoa wa Geita Comrade Adamu Paul Ndalawa   amewasihi wanachama hao kujenga tabia ya kushirikiana kwa umoja ili chama kiendelee kuwa na nguvu na kuwahamasisha kujitokeza kugombea nafasi mbalimbali ndani ya chama huku akiwaonya wasimamizi wa uchaguzi kutojenga tabia ya kubagua watu wa kugombea kulingana na makundi au ujamaa walionao ili kunusuru maslahi ya chama na taifa kwa ujumla.

Comments