Mhe. Doto Biteko awaangalia Vijana wa Bukombe kwa macho mawili.


Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi(CCM) Kata ya Katente  Comrade Daniel Machongo akizungumza na wananchi wa Mtaa wa Bwenda Namba1 katika mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisalimiana na baadhi ya wadau wa Kata ya Katente waliohudhulia katika mkutano huo.





Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani  Geita,Mhe. Doto Mashaka Biteko
amewataka wananchi wa Mtaa wa Bwenda   Kata ya Katente hasa  vijana kuachana na  siasa zisizo na tija huku akiwasilihi kushiriki  katika kujiletea maendeleo kwa ujumla na kwa mtu mmojammoja kutokana na rasilimali walizonazo.


Mhe.  Biteko aliyasema hayo kwenye mkutano wa Hadhara uliofanyika Mtaa wa Bwenda  Kata ya Katente  alipokwenda kuonana na  wananchi ili kujadiliana shughuli za maendeleo  na kusikiliza kero zao.

Alisema inahitajika nguvu ya pamoja ili kuhakikisha wana maliza changamoto za eneo hilo, zikiwemo ukosefu wa miundo mbinu ya barabara, kituo cha Afya, miradi ya maji na kuzorota kwa ufaulu wa wanafunzi na kuwaomba wazazi kushirikiana na walimu kwa kufuatilia kwa karibu zaidi maendeleo ya vijana mashuleni.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko alisema yupo tayari kushirikiana na vijana hao katika kujikwamua na wimbi la umaskini huku akiwasihi vijana hao na Jimbo zima kwa ujumla kujiunga katika vikundi na kuwaahidi kuleta milioni hamsini na moja kwa ajili ya kuwainua vijana kwa kuanzisha na kuboresha shughuli mbali mbali wanazozifanya kwa ajili ya  kujipatia kipato kwa umoja wao bila kujali itikadi,dini wala ukabila .

Comments