Mbunge wa Jimbo la
Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizumgumza na wafanyabiashara wa Kata ya Uyovu.
Mmoja wa wafanyabiashara hao alieuliza maswali katika mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Uyovu Dkt John Fabiani Ng'home akizungumza kwenye mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko alipokutana na wafanya biashara wa Kata ya Uyovu nakuwaeleza Kituo hicho cha Afya kinawahudumia wagonjwa wengi hasa wazee,watoto na wamama wajawazito ambao hutibiwa bure na kumwomba Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb) kuishinikiza Serikali kupandisha Hadhi Kituo hicho cha Afya.
Wafanyabiashara wa Uyovu Wilayani Bukombe Mkoa wa Geita wamekutana na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko na kumweleza umuhimu wa sekta hiyo na changamoto zao.
Pia
wamemweleza Mbunge huyo kuwa pamoja na kuchangia serikali maendeleo kwa kulipa
kodi hawanufaiki na fedha zao hizo kutokana na serikali kutotengeneza
miundombinu ya barabara hasa Kitongoji
cha Azimio na huduma ya umeme kufikia
watu wachache sana hali inayo wanyima fursa ya kuboresha biashara zao.
Kwa
majibu ya Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb) aliwaeleza wafanyabiashara hao kuwa
umeme uliosambaa kwa sasa sio wa mradi wa REA nakusema mradi huo ulikuwa
unaitwa UMEME NAMBA 5 uliokuwa unafadhiliwana na Banki ya maendeleo ya Afrika(ADB)
na kuwaomba wawe na subira kwani Wilaya nzima na viunga vyake vimeingizwa
kwenye mradi wa REA na kuwahakikishia kumaliza changamoto ya umeme kabisa
Pia
aliwasihi wafanyabiashara hao kuachana na siasa na badala yake wawe kipaumbele
kwa kuibua miradi ya maendeleo ili waweze kupata fedha za ruzuku kutoka
serikalini ili kuharakisha maendeleo kwa mmoja mmoja na kwa ujumla.
Comments
Post a Comment