Ushirombo Rangers yamliza Runzewe Academy - michuano ya GEREFA



 Wachezaji wa Timu ya Ushirombo Rangers kwa pamoja wakipanga mikakati ya Ushindi.


Wachezaji wa  Timu ya Runzewe Academy wakijadiliana nini kifanyike dhidi ya wapinzani wao.

 Mwamzi wa Mchezo akitoa kadi ya NJANO kwa Masanja Sabuka wa Timu ya Runzewe Academy kwa kumfanyia Madhambi  Juma Mbelele ambaye ni Mchezaji wa Timu ya Ushirombo Rangers.




 Kama kawaida yao Mashabiki.

 Katibu wa Chama Cha Mpira Wilaya ya Bukombe (BUFA) Bw. Bosco Midadi akiwa na baadhi ya wadau wa soka Wilayani humo wakitazama juhudi za wachezaji dimbani.
  
Baadhi ya Mashabiki wakiwa katika umakini wa kufuatilia Mchezo.


 Timu ya Ushirombo Rangers  imeibuka kidedea dhidi ya Timu ya Runzewe Academy kwa kuichapa gori moja  bila kwenye viwanja vya Runzewe Stadium katika michuano inayoendelea ya ligi daraja la tatu ngazi ya Mkoa inayoratibiwa na  Chama Cha Mipira wa Miguu Mkoa wa Geita (GEREFA)  .

Mechi ya kwanza ya timu hizo imechezwa na iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki katika uwanja wa Runzewe Statium ambapo Timu ya Ushirombo Rangers iliichapa gori 1 Timu ya Runzewe Academy  dakika ya 82  kupitia kwa kiungo mshambuliaji Nestory Jamhuri. 

Hadi dakika ya tisini ya mchezo huo Timu ya Runzewe Academy haikupata hata gori la kufutia chozi.

 Kipa wa Ushirombo Rangers  Fadhili Selemani  ndiye aliyekua nyota wa mchezo kwa kuokoa mipira mingi ya hatari likiwemo shuti la Athony Mwalyoyo alilopiga ndani ya 18 na kipa huyo wa Ushirombo Rangers kuiokoa kwa juhudi kubwa .

Comments