RAIS DKT. MAGUFULI AMSAIDIA DADA NEEMA MWITA WAMBURA ALIYEMWAGIWA UJI WA MOTO NA MUMEWE MKOANI MARA.

Dada
Neema Mwita Wambura (32) akizungunza na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia njia ya Simu akimshukuru kwa
msaada aliompatia wa kufanyiwa tena uchunguzi wa afya yake katika
hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Pia Rais Dkt. Magufuli ameahidi
kumpatia hifadhi mama huyo pamoja na watoto wake watatu ambao kwa sasa
wapo Bunda mkoani Mara. Pia Rais Dkt. Magufuli alimpatia msaada Dada
huyo kiasi cha Shilingi laki tano. Dada Neema Mwita Wambura aliungua
vibaya mara baada ya kumwagiwa uji wa moto uliokuwa unachemka jikoni na
mume wake katika kijiji cha Kyagata, Tarime mkoani Mara.
Mama
Mjane Mariam Amir ( Bibi Mwaija ) ambaye amempa hifadhi Neema Mwita
Wambura nyumbani kwake Tandika Davis Corner akiomba dua kumuombea Rais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kupitia njia
ya Simu kumshukuru mara baada ya kuzungumza naye kuhusiana na kumsaidia
Dada Neema Mwita Wambura (32). Rais Dkt. Magufuli amempongeza Mama huyo
Mjane ambaye ameonesha moyo wa kizalendo na kumpa hifadhi Dada huyo
aliyemwagiwa uji wa moto na mumewe katika kijiji cha Kyagata, Tarime
mkoani Mara. Pia Rais Dkt. Magufuli alimpa Mjane huyo kiasi cha Shilingi
laki tano.
Dada
Neema Mwita Wambura (32) wakwanza kulia akiwa pamoja na Mama Mjane
Mariam Amir ( Bibi Mwaija ) wakiwa ndani ya gari mara baada Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kumsaidaia ili
aweze kufanyiwa tena uchunguzi wa afya yake katika Hospitali ya Taifa ya
Muhimbili jijini Dar es Salaam.
Wauguzi
wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili wakimpokea Dada Neema Mwita Wambura
(32) na kuanza mara moja kumfanyia tena uchunguzi wa afya yake katika
majeraha aliyoyapata mara baada ya kumwagiwa uji wa moto uliokuwa
ukichemka jikoni kitendo kilichofanywa na mume wake.
Mkurugenzi
Mkuu wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Profesa Lawrence Museru
akimjulia hali Dada Neema Mwita Wambura (32) mara baada ya kufikishwa
tena hospitalini hapo. Dada Neema Mwita alifanyiwa upasuaji mara nne
katika siku za nyuma hospitalini hapo Muhimbili ili kutibu majeraha yake
hayo ya moto.
Daktari
Bingwa wa magonjwa ya dharura na Ajali katika hospitali ya Taifa ya
Muhimbili Dkt. Juma Mfinanga akizungumza kuhusu hali ya mgonjwa Dada
Neema Mwita Wambura (32) aliyefikishwa tena katika Hospitalini hapo kwa
ajili ya uchunguzi wa Afya yake.
Dada
Neema Mwita Wambura (32) akiwa katika hali ya majonzi kufatia majeraha
makubwa mwilini mwake kufatia kumwagiwa uji wa moto na mume wake mkoani
Mara.
Daktari
Bingwa wa upasuaji wa ngozi kutoka Hospitali ya Taifa ya Muhimbili Dkt.
Ibrahim Mkoma akizungumzia historia ya mgonjwa huyo ambaye yeye pamoja
na jopo la madaktari bingwa walimfanyia upasuaji ili kutibu majeraha
yake ya ngozi katika kipindi cha nyuma. PICHA NA IKULU
Comments
Post a Comment