Kushoto
ni Mtanzania aliyejulikana kwa jina la Pamela David Kirrita (41) akiwa
na mwanamke mwingine raia wa Zambia Thelma Mkandawire (38) wakiwa
mbaroni kwa tuhuma za kukutwa na kilo 4 za madawa ya kulevya aina ya
cocaine katika hoteli moja kusini mwa jiji la New Delhi, India.
Naibu
Mkurugenzi Mkuu wa kikosi cha kupambana na madawa ya kulevya cha New
Delhi (NCB) Rajinder Pal Singh amesema watuhumiwa walikamatwa katika
hoteli iliyopo eneo la Mahipalpur jana Februari 4, 2017.
“Baada
ya kupata taarifa kutoka vyanzo vyetu, timu yetu ikatega mtego kwa
Mkandawire aliyewasili uwanja wa ndege wa kimataifa wa Indira Ghandi
akitokea ughaibuni akiwa na mzigo huo.
“Baada
ya kuchekiwa uwanjani pale aliondoka na taxi hadi hotelini. Timu yetu
ilimfuatilia na kumuona mara alipofika hotelini akakutana na Pamela
David Kirrita aliyekuwa aupokee huo mzigo”, alisema Mkurugenzi wa NCB
tawi la New Delhi.
Amesema
walipohojiwa Kirrita alibainisha kuwa alikuwa akiishi katika hoteli
moja katika kitongoji kiitwacho Vasant Kunj tokea Januari, na kwamba
alikuwa na mawasiliano na mtu mwingine raia wa kigeni ambaye ndiye
angempasia mzigo baada ya kuuchukua toka kwa Mkandawire.
Polisi
wanasema mzigo ulifichwa kwenye uwazi wa begi la safari, na kwamba
Mkabdawire aliwahi kukamatwa nchini Pakistani mwaka 2015 na kukaa
mahabusu kwa zaidi ya miezi sita, huku Pamela akikiri kutembelea India
zaidi ya mara sita tokea mwaka 2006.
Kwa
sheria za India, mshtakiwa atayekutwa na hatia ya madawa ya kulevya
yaliyokuwa ya kibiashara ni kifungo cha kati ya miaka 10 ama 20 gerezani
na faini ya Rs 1 lakh (sawa na dola za Kimarekani 15,000) ama Rs 2
lakhs (dola 3000).
Comments
Post a Comment