Shule ya Sekondari iliyoko Kata ya Busonzo inayotegemea kufunguliwa.
Nyumba za Waalimu wa Shule hiyo iliyoko Kata ya Busonzo katika hatua za awali (msingi).
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko na msafara wake wakitokea Shule ya Msingi Narusunguti baada ya kuzungumza na waalim pamoja na uongozi wa Shule hiyo.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Narusunguti.
Wananchi wa Kijiji cha Narusunguti wakiwa katika umakini zaidi wa kumsikiliza Mbunge wao
Hawa ni baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Narusunguti waliojiteza kuuliza maswali katika mkutano wa Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb).
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akimkabidhi mipira mmoja wa waalimu wa Shule hiyo ya msingi Narusunguti baada ya ombi lao.
Mbunge wa jimbo la Bukombe Mkoani Geita,Mhe. Doto
Mashaka Biteko
amewaomba wananchi kuacha vitendo vya kuendekeza siasa wakati wa
kutekeleza shughuli za maendeleo zinapo ibuliwa kuanzia ngazi ya Kijiji ili kujiletea mandeleo kwa haraka.
Biteko aliyasema hayo wakati wa ziara yake katika Kijiji cha Narusunguti Kata ya Busonzo alipokwenda kuwashukuru wananchi kwa kumchangua na kuhamasisha kuibua
miradi ya maendeleo kwani Wilaya ya Bukombe iko nyuma kimaendeleo
kutokana na wananchi kuendeleza siasa hali ambayo imesasabisha bara
bara nyingi hazijafunguliwa, huduma za Afya zisizo endana na mahitaji
ya watu kutokana na upungufu wa Zahanati.
amewaomba wananchi kuacha vitendo vya kuendekeza siasa wakati wa
kutekeleza shughuli za maendeleo zinapo ibuliwa kuanzia ngazi ya Kijiji ili kujiletea mandeleo kwa haraka.
Biteko aliyasema hayo wakati wa ziara yake katika Kijiji cha Narusunguti Kata ya Busonzo alipokwenda kuwashukuru wananchi kwa kumchangua na kuhamasisha kuibua
miradi ya maendeleo kwani Wilaya ya Bukombe iko nyuma kimaendeleo
kutokana na wananchi kuendeleza siasa hali ambayo imesasabisha bara
bara nyingi hazijafunguliwa, huduma za Afya zisizo endana na mahitaji
ya watu kutokana na upungufu wa Zahanati.
Mbunge aliwaomba wananchi waungane kujitolea kujenga
darasa la shule ya msingi Narusunguti na kuwaahidi kuwaletea mabati ya kupaulia
darasa hilo ili kupunguza adha ya watoto kusoma katika hali ya mbanano na kuwasababishia
kufanya vibaya kimasomo katika mtihani wa darasa la saba kwa kuwa wa tatu
kutoka mwisho kati ya shule 75 za Wilayani humo.
Wakati akibainisha mafanikio kwa Wilaya ya Bukombe kwa
sasa alianza kwa kuwapongeza wanaNyarusunguti kwa kumaliza kabisa changamoto ya
madawati katika shule hiyo na kuwasihi kuongeza ushirikiano kwa waalimu ili
kuongeza ufaulu wa watoto hao.
Pia aliwasihi wakazi hao kuwajengea utamaduni wa kusomesha
watoto wao kwani shule ya sekondari ya Busonzo imekaribia kufunguliwa ili ianze kutoa huduma ya elimu na kutoa
fedha kwa ajili ya ujezi wa vyoo ili kuharakisha uanzishwaji wa shule hiyo.
Mhe Biteko alisema kwa kushirikiana na serikali barabara ya Namparahara hadi Msonga itaanza kukarabatiwa hivi karibuni na tayari fedha zimekisha tolewa ili kuboresha miundo mbinu hiyo na kuongeza vituo vya Afya na Zahanati ili kuondoa chamgamoto za kutembea umbali mrefu kutafuta huduma za Afya.
Awali mkazi wa Kijiji cha Narusunguti Nduta Ngasa alisema kuwa kutokana
na Kata hiyo kutokuwa na huduma muhimu ya shule ya sekondari na
Zahanati wanafunzi na wananchi wamekuwa wakipata changamoto
ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata huduma hizo na kumwomba Mhe. Doto Mashaka Biteko (Mb) kuitatua changamoto hizo za maji katika Kata hiyo ili kuwanusuru wakazi wa maeneo hayo.
na Kata hiyo kutokuwa na huduma muhimu ya shule ya sekondari na
Zahanati wanafunzi na wananchi wamekuwa wakipata changamoto
ya kutembea umbali mrefu kwenda kupata huduma hizo na kumwomba Mhe. Doto Mashaka Biteko (Mb) kuitatua changamoto hizo za maji katika Kata hiyo ili kuwanusuru wakazi wa maeneo hayo.
Comments
Post a Comment