Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekieli Kyunga (wa pili kushoto) Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mhe. Josephat Maganga (wa kwanza kushoto),Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe na Diwani wa Kata ya Busonzo Mhe. Safari Nikas Mayala (katikati) na kulia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko wakiwa katika umakini wa kupitia makablasha ya kikao.
Mwenyekiti wa Kamati ya Afya Elimu na Maji Mhe. Juma Lushiku (kushoto) anaemfuata ni Mwenyeki wa Kamati ya maadili Mhe. Lozaria Masokola na kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mzingira Mhe. Lameck Warangi
Mwenyekiti wa Kamati ya Afya Elimu na Maji Mhe. Juma Lushiku (kushoto) anaemfuata ni Mwenyeki wa Kamati ya maadili Mhe. Lozaria Masokola na kulia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Uchumi Ujenzi na Mzingira Mhe. Lameck Warangi
Baadhi ya Madiwani nao kwa umakini mkubwa wakipitia makablasha.
Picha ya Baadhi ya Watumishi katika Wilaya ya Bukombe.
Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Kyunga akizungumza na wajumbe wa Baraza hilo la Madiwani.
Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe
Mkoani Geita wamemuomba Mkuu wa Mkoa Geita Meja Jenerali Ezekieli Kyunga kuinua wakulima
wa mazao ya chakula na biashara kwa kuwasaidia kuwatafutia wadau wenye uwezo wa
kuwaletea pembejeo sahihi ili wakulima hao waepukane na hasara zitokanazo na
dawa zisizoweza kuuwa wadudu waharibifu wa mazao,
Sambamba na kumwomba Mkuu huyo kuzidisha mkuzo kwa
kushilikiana na Wakuu wa Wilaya katika kuhakikisha Chakula hakiuzwi nje ya Mkoa
wa Geita kutokana na kuzidi kwa ukame katika msimu wa mwaka huu.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya Madiwani hao Mhe. Eric Kagoma na Juma Lushiku
wamesema kuwa wamekuwa wakicheleweshewa
pembejeo za kilimo huku zingine zikiwa haziwauwi wadudu hao kabisa hali
inayowakwamisha katika uzalishaji wa bidhaa zinazotokana na kilimo cha mazao.
Katika hatua nyingine Mhe. Lushiku amemuomba Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Mstaafu
Ezekiel Kyunga kujua idadi halisi ya chakula kilichopo na mahatiji ya watu kwa
sasa na kuviomba vyombo vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha
zao la chakula hali toki nje ya Mkoa.
Lushiku aliwataka Madiwani hao kuongeza bidii ya kutoa ushirikiano wa
kutosha kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili kupunguza matukio mbalimbali ya
uharifu yanayoripotiwa kutokana na hali ngumu itokanayo na ukame .
Pia Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko aliwaomba madiwani
kutoa elimu kwa wananchi juu uvunjaji wa sheria na kuwasihi watumishi wa idara
mbalimbali katika Wilaya hiyo kufanya kazi ya kuwahudumia wananchi bila ubaguzi
na unyanyasaji wa aina yeyote.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Geita Meja Jenerali Ezekieli
Kyunga alisema atahakikisha anatoa ushirikiano wa kutosha kwa viongozi wa ngazi
zote ili kuleta maendeleo ya Wilaya,Mkoa na Taifa kwa ujumla
Mhe. Kyunga aliwataka
viongozi hao kuzidisha ubuni na utafiti ili kumaliza changamoto katika
jamii ikiwa ni pamoja na kuendeleza ulinzi shirikishi,kujenga maghala ya
kuhifadhia chakula kama Wilaya,kujenga tabia ya kufanya biashara baina ya kata
na kata, Wilaya na Wilaya ili kuunusuru Mkoa na balaa la njaa.
Comments
Post a Comment