LIGI DARAJA LA NNE KUANZA KUCHEZWA BUKOMBE.


 Timu zikielekea waliko wasimamizi wa mchezo tayari kwa ukaguzi na
wenye jezi nyekundu ni Timu ya Eleven King Fc na waliobaki ni Wachezaji wa Timu ya Rufuna Fc.

  Mwamuzi wa ndani ikifanya utambulisho kwa viongozi wa Chama cha mpira Wilaya ya Bukombe (BUFA),na mwenye Shati nyeupe ni Katibu BUFA bw. Bosco Mwidadi anafuata ni Mtunza Hazina wa BUFA bw. James Malima.  




 Mashabiki kama kawaida yao


Timu ya Rufuna Fc iliyoko  Kata ya Katente Wilayani Bukombe Mkoani Geita jana imejinyakulia  ushindi wa gori 1-0 dhidi ya Timu ya Eleven King Fc iliyoko Kata ya Bulega kwenye ufunguzi wa ligi daraja la nne inayosimamiwa na Chama cha Mpira Wilaya Bukombe (BUFA)iliyoanza jana katika viwanja vya Bulega .

Mechi hiyo iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki katika uwanja wa Bulega Timu ya Rufuna Fc iliichapa gori 1 bila Timu ya Eleven King Fc dakika ya 43  kupitia kwa kiungo mshambuliaji Nestor Jamhuli.
Hadi dakika tisini ya mchezo huo Timu ya      Eleven King fc haikupata hata gori la kufutia machozi.

wakati akizungumza katibu wa chama cha mpira wilaya ya Bukombe Bw. Bosco kwenye ufunguzi wa  ligi hiyo aliwaeleza  wachezaji na mashabiki kuwa lengo la ligi hiyo ni kukuza vipaji vya vijana kimichezo hivyo haina haja ya ugomvi ndani na nje ya uwanja huku akiwasihi wananchi wa Bukombe na viunga vyake kujitokeza kwa wingi kutazama ligi hiyo ili kuwatia hamasa vijana wanao shiriki katika ligi hiyo. 
 
 Kwa upande wake kocha wa timu ya  Rufuna Fc bw. Benjamini Rufuna Ntoro amewashukuru wachezaji wake kwa ushindi walioupata na kuwataka kuendelea kufanya mazoezi kwa bidii ili  kufika  waendelee kufanya vizuri katika mechi ijayo ya marudiano na kujichukulia ushindi tena. 

Nae katibu wa timu ya Eleven King bw. Nestory Machibya aliyapokea matokeo hayo ya kushindwa na kuwataka wachezaji hao kutokata tamaa kulingana na kushindwa kufikia malengo yao.

Comments