Watoto waliopondwa na jengo la Kanisa la TAG Namonge wanusurika

Picha ya Kanisa la Tanzania Assembles of God (TAG) Namonge lililoezuliwa na mvua kubwa ilioambatana na upepo mkali na kusababisha majeruhi.


 Katibu Tawala wa Wilaya ya Bukombe Bw. Paul Cheyo akiwajulia hali wagojwa waliopondwa na jengo la Kanisa la Tanzania Assembles of God (TAG) Namonge lililoezuliwa na mvua kubwa iliyoambatana na upepo katika Kijiji cha Namonge. 

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Bukombe Bwn. Dionis Myinga akizungumza na mmoja wa wagonjwa hao waliokuwa wamelazwa katika Kituo cha Afya Uyovu kwa matibabu.

Mganga wa Kituo cha Afya Uyovu Dk Joshua Mazengo

Mganga wa zamu Kituo cha Afya Uyovu Dk  Joshua Mazingo alisema alipokea wanafunzi  watatu  Thimoseo Sospiter (12) akiwa amechanika kwenye kidevu ,Adiriano Mihambo (14) akiwa ameumia kwenye mguu  na  anaedelea na uchunguzi kubaini kama amevunjika mguu.
Dk Mazingo  aliwataja wengine ambao walikuwa na majeraha ni Heppy Sospiter (10) na mtoto ambaye hasomi  Daud Charles (6) mganga wa zamu alisema aliwapokea tarehe 16/11/2016majira ya saa 1:00 usiku na kuwapatia huduma na hali zao zinaedelea vizui.


Comments