Taarifa iliyotoka Ikulu ya White House baada ya ushindi wa Donald Trump


Taarifa iliyotolewa leo November 9 2016 na Ikulu ya Marekani baada tu ya ushindi wa Donald Trump imeeleza kuwa Rais Obama amempigia simu Donald Trump kumpongeza kwa ushindi wake katika uchaguzi wa Urais ambapo pia amemwalika ikulu ya White House mnamo Alhamisi kuzungumza naye.
Obama pia amempigia Hillary Clinton na kumpongeza kutokana na alivyofanya kampeni zake, aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa Rais Obama atatoa taarifa zaidi Jumatano kutoka White House kujadili matokeo ya uchaguzi na hatua ambazo wanaweza kuchukua kama taifa kuungana tena pamoja baada ya kipindi cha uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkali

Comments