Taarifa
iliyotolewa leo November 9 2016 na Ikulu ya Marekani baada tu ya ushindi
wa Donald Trump imeeleza kuwa Rais Obama amempigia simu Donald Trump
kumpongeza kwa ushindi wake katika uchaguzi wa Urais ambapo pia
amemwalika ikulu ya White House mnamo Alhamisi kuzungumza naye.
Obama pia
amempigia Hillary Clinton na kumpongeza kutokana na alivyofanya kampeni
zake, aidha taarifa hiyo imeeleza kuwa Rais Obama atatoa taarifa zaidi
Jumatano kutoka White House kujadili matokeo ya uchaguzi na hatua ambazo
wanaweza kuchukua kama taifa kuungana tena pamoja baada ya kipindi cha
uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkali
Comments
Post a Comment