Mhe. Doto Mashaka Biteko(Mb) asema na Wananchi wa Kakoyoyo

  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mshaka Biteko akisaini kitabu cha wageni tayari kwa kuaanza mkutano

Mmoja ya Kikundi kilichotoa Burudani(Waswezi) 

  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mshaka Biteko na Diwani wa Kata ya Bulega wakivituza vikundi vilivyotoa burudani katika Mkutano huo 

Picha ya Wanakwaya wa Kikundi cha  Hamasa wakitoa Burudani katika mkutano wa Mbunge 

Picha ya msanii machachari wa Kijiji cha Kakoyoyo aliyeimba wimbo wenye ujumbe wa kuomba daraja.

Diwani wa Kata ya Bulega akisema na wakazi wa kijiji cha Kakoyoyo

 
 Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mshaka Biteko akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Kakoyoyo Kata ya Bulega.

 

Wananchi wakisikiliza kwa makini Mbunge wao



 Wananchi wa Kijiji cha Kakoyoyo, Kata ya Bulega , Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita wamemuomba Mbunge wa Jimbo la Bikombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kushirikiana na wafugaji kwa kuihimiza serikali kuwatengea maeneo ya malisho hasa nyakati za kilimo zinapoanza.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya Wananchi hao Bw Magesa Malima na Malingumu Juma wamesema kuwa  wananchi  katika Wilaya hiyo wamekuwa wakihangaika sana kutafuta maeneo ya malisho  hali inayowakwamisha katika upatikanaji wa maeneo ya maji na chakula cha mifugo yao pa kudumu hivyo kuwasababisha uchumi wao kuzorota sana.

Katika hatua nyingine Bw Malingumu Juma amemuomba Doto Mashaka Biteko(Mb) kutoa ushirikiano kwa wananchi kwa kuisukuma serikali katika swala zima la huduma ya maji ya uhakika katika Kijiji cha Kakoyoyo pamoja na vijiji jirani ndani ya Kata hiyo ya Bulega,kusaidia ajira kwa vijana,upungufu wa walimu wa Shule za Kakoyoyo na kumsihi Mbunge huyo aisukume halmashauri ili iwaletee huduma ya mabarabara ya mitaa kwani wao wako katika halmashauri ya mji mdogo.

Aidha Mbunbe wa jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko amesema atahakikisha anatoa ushirikiano wa kutosha kwa wananchi hao hasa katika maswala ya kuiweka Wilaya kuwa na miundo mbinu ya mabarabara mizuri na kuwaeleza mikakati inayo endelea dhidi ya barabara zao ikiwemo  kuzipandisha hadhi kutoka barabara zinazohudumiwa na mfuko wa halmashauri hadi kuwa barabara zinazohudumiwa na wakala wa Barabara Mkoa (Tanroads) na huwasihi wananchi kufuga kisasa kwa kupunguza idadi ya mifugo ili kupunguza adha zianazo jitokeza wakati huu ambao serikali ikipitia maeneo yake upya kipita Wizara zenye dhamana. 

Comments