Mchungaji Jonathan Kasase akifungua mkutano kwa maombi
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na Wachungaji wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) Tarafa ya Siloka.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akijichotea baraka kwa kuwanawisha watumishi wa Mungu.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akiwa na viongozi wa Umoja wa Makanisa ya Kipentekoste (CPCT) Tarafa ya Siloka.
Picha ya Pamoja baada ya mkutano.
Mbunge wa Jimbo la
Bukombe Mkoani Geita Mhe,Doto Mashaka Biteko amekutana na wachungaji wa Umoja
wa Makanisa ya Kipentekoste(CPCT) wa Tarafa ya Siloka na kufanya mazungumzo nao
sambamba na kutoa shukrani za dhati kwa uhamasishaji wao kwenye ushindi wake na
kuwaahidi kutenda haki ya kusimamia ukweli tu na kuwawakilisha katika Bunge la
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kupeleka mawazo yao hivyo wamuunge mkono
kwa kumuombea.
Aidha katika mkutano huo
Wachungaji waliorodhesha changamoto zao ikiwa ni pamoja na miundo mbinu duni ya
barabara,ukosefu wa kituo cha afya sambasamba na dawa na mifuko ya kutunzia
damu hali inayosabaisha vifo visivyo vya lazima kwa waumini wao, kucheleweshewa
pembejeo za kilimo hali inayowakwamisha katika uzalishaji bidhaa zinazotokana na kilimo cha mazao na
kusababisha uchumi wao kuyumba.
Aidha Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto
Biteko amewaomba Wachungaji hao wajitahidi kuwasaidi vijana kuwa na hofu ya
Mungu na kufanya kazi kwa bidii ili kulinusuru taifa na kwasihi waumini wao na
jamii inayowazunguka kwa ujumla kufanya kazi kwa kila mtu katika eneo lake ili
kuharakisha maendeleo.
Comments
Post a Comment