Walimu wa Bukombe waadhimisha siku ya Mwalimu Duniani 2016

Meza kuu tayari kwa Sherehe


Wageni waalikwa wakiwa katika nafasi zao

 Mmoja wa walimu katika maadhimisho hayo akichambua uzuri na changamoto za ualimu.

 Hawa ni walimu wakiwa wamepita mbele katika madhimisho hayo kwa ajili ya kutoa Burudani wakiongozwa na Mama Mstaafu ambae jina lake halikuweza kutambulika kwa haraka .

 Huyu ndiye mshindi wa kwanza akipewa zawadi ya fedha na  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko ambae kwa siku hiyo alikuwa mgeni maalum na kuandaa mpambano huo wa Burudani ya Kucheza. 

 Picha ya Mwalimu Anathory Kubi kizungumza  ambaye ndiye aliye kuwa anaagwa baada ya kumaliza kipindi chake kutumikia serikali akiwa mwalimu ndani ya siku hiyo ya maadhimisho ya mwalimu duniani

 Picha ya Pamoja ya walimu aliokuwa akifundisha nao katika  shule ya msingi Ibamba kabla hajastaafu.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza wakati akitoa zawadi kwa mstaafu Mwl Anathory Kubi 




Leo(jana) ikiwa ni siku ya walimu duniani,Walimu wa Kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka Wilaya Bukombe Mkoani Geita wameungana Walimu Duniani katika  maadhimisho  ya mwaka huu yameangukia ndani ya ajenda ya maendeleo endelevu ya 2030(SDG’s) iliyoafikiwa mwaka mmoja uliopita..
Maudhui ya mwaka huu ni “Thamini Walimu, Boresha Hali zao”, yanajumuisha kanuni za msingi kuhusu ustawi wa walimu zilizopitishwa miaka 50 iliyopita kwa ushirikiano baina ya UNESCO na Shirika la Kazi Duniani(ILO), na pia yanamulika lengo nambari nne katika ajenda ya maendeleo ya “Kuhakikisha elimu bora, shirikishi na yenye usawa na inayojenga fursa ya maisha ya kujifunza kwa wote”.
Akizungumza katika  maadhimisho hayo yaliyojumuishwa na kumwaga mstaafu Mwalimu Anathory Kubi,  Mwalimu Doto Mashaka Biteko ambae pia ni Mbunge wa Jimbo la Bukombe  amesema ni siku ya furaha sana kwa walimu maana huinua hali ya kufanya kazi na huwavutia watoto wengi kuipenda kazi ya ualimu na kuwa sisitiza waalimu kuhakikisha kutohawajihusishi na vitendo vya ulevi, rushwa na hata kuwa na mahausiano ya mapenzi na wanafunzi mambo haya yanapotendeka yanatupunguzia hadhi kwa jamii na kujenga taifa lisilo na nidham pia aliwataki  walimu wenzake siku njema ya mwalimu duniani.

Kwa upande wake Mwalimu mstaafu Anatory Kubi amesema kuwa ni muhimu Walimu  washirikiane kwa kila namna kumwondoa adui yetu mkubwa ujinga, maradhi na magonjwa. Na kuongeza kuwa  maadui wote hawa huondolewa kwa urahisi na Elimu ambayo sisi ndo tunaoitoa kwa watoto wa Taifa letu.

Comments