Ikiwa ni mwedelezo wa Ligi ya Doto Cup ngazi ya Wilaya baada
ya kushindana Vijiji kwa Vijiji, Kata kwa Kata, Tarafa kwa Tarafa,Timu ya Uyovu
Fc iliyopo Kata ya Uyovu Wilayani
Bukombe Mkoani Geita jana ilifanikiwa kuichapa gori 4-2 Timu ya Ketente Fc katika hatua
ya mzunguko wa kwanza wa Ligi hiyo ngazi ya Wilaya.
Mechi hiyo iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki katika uwanja
wa Halmashauri ya Bukombe ulioko Kilimahewa Kata ya Katente
Timu ya Uyovu Fc
iliichapa gori 4 Timu ya Katente Fc ikiwa ni dakika ya 8 kwa mchezaji Welason Ramadhani
mwenye jezi namba 10,gori la pili na la nne lilifungwa na kiungo mshambuliaji
Rashid Suleiman mwenye jezi namba14 ikiwa ni dakika ya 13 na 73 nala tatu
kufungwa na mchezaji Ramadhani Unus mwenye jezi namba 8 dakika ya 23
Kwa upande wao Katente Fc katika harakati za kujikwamua
walipata magori mawili kupitia kwa mchezaji Matendo Ngai mwenye jezi namba 4
dakika ya 18 na dakika ya 38 kujipatia gori la pili kupitia kwa kiuongo
mshambuliaji Lenard Kumuhu mwenye jezi namba 9 hadi dakika ya tisini jitihada
zao zilikomea hapo na kukubali matokeo.
Akizungumza baada ya
mechi kumalizika, Katibu wa Chama cha
Mpira Wiayani Bukombe (BUFA) Mwl Kabalega amezipongeza timu zote zilizojitokeza
kushiliki ligi hiyo iliyoandaliwa na
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa lengo la kuendeleza vipaji vya
vijana wanaopatikana ndani ya jimbo la Bukombe.
Comments
Post a Comment