Mhe. Doto Biteko akutana na uongozi wa Shule ya Msingi Ibamba

  Shule ya Msingi Ibamba.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe,Doto Mashaka Biteko(mwenye tishetiya mistari)na Afisa elimu Wilaya ya Bukombe Bw. Kabanga wakisaini kwenye vitabu vya wageni katika Shule ya Msingi Ibamba.




 Hali halisi ya wanafunzi wa darasa la nne katika shule ya msingi Ibamba. 

  Mhe,Doto Mashaka Biteko(Mb) akiwatia moyo  wanafunzi wa shule ya msingi Ibamba wanaosomea nje kutokana na ukosefu wa madarasa ya kutosha.

  Mhe,Doto Mashaka Biteko(Mb) akiwa na uongozi wa shule ya msingi Ibamba pamoja na watalamu kutoka Wilayani wakijadiliana tayari kwa kuanza ujenzi wa vyumba vya madarasa na matundu ya vyoo shuleni hapo.




Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe,Doto Mashaka Biteko amekutana na uongozi wa shule  ya msingi Ibamba iliyoko Kata ya Uyovu Tarafa ya Siloka Wilayani Bukombe ikiwa ni hatua ya usimamizi wa fedha zilizotolewa na Serikali kwa lengo la kujenga vyumba vya madarasa 8 na vyoo 20 vitakavyo gharimu kiasi cha Tsh. 194,000,000/=.

 Katika hatua hiyo Mhe. Biteko aliwasihi viongozi wa shule wajitahidi kutoa elimu kwa jamii ili wazazi waongeze bidii ya kuwahudumia watoto wao kwa kuwanunulia vifaa vya shule kwa wakati ili kushirikiana na serikali inayotoa elimu bure  na kuwasihi wananchi hao kuachana na siasa za kukwamisha  maendeleo na kuwaambia wafanye kazi  kwa kushirikiana na viongozi wao bila kujali itikadi zao dini wala ukabila ili kuinua elimu ya shule, wilaya na taifa kwa ujumla  na kusema kuwa wakati wa siasa sio huu. 

 



Comments