Fainali ya Ligi ya Doto Cup 2016



 Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akifungua michuano ya Ligi ya Doto Cup Fainali ngazi ya Wilaya katika Uwanja wa Kilimahewa uliyoko Mjini Ushirombo.
   

Moja ya mchezo wa kuvuta Kamba ukiwa ni miongoni wa bonanza katika Ligi hiyo.

Mashabiki wa CCM wakishangilia ushindi wao baada ya bonanza la kuvuta kamba kati ya Wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Vs Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hatimaye CCM kuibuka kidedea na kupewa Zawadi ya Mbuzi na Chadema kupewa Kiasi cha Tsh. elfu ishirini ikiwa ni moja ya mabonanza katika Ligi hiyo ya Doto Cup.

  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko ikikadhi Zawadi kwa wanachama wa CCM baada ya kuwashinda wanachama wa CHADEMA katika mchezo wa kuvuta kamba ikiwa ni moja ya bonanza ndani ya Fainali ya Doto Cup

Washindi wa Mchezo wa kuvuta Kamba(WanaCCM) wakiwaonyesha mashabiki Zawadi yao baada ya kukabidhiwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.

Wanachama wa CHADEMA wakiwa jukwaani tayari kwa kupokea zawadi yao baada ya kushiriki mchezo wa kuvuta kamba na kushindwa na WanaCCM na kupata Elfu Ishirini  kutoka kwa   Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.

Picha ya waamuzi wa Michezo wakipokea zawadi ya usimamizi mzuri wa mechi kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko



 Viongozi wa Timu ya Namsega wakipokea zawadi ya mshindi wa tatu Ligi ya Doto Cup kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.


  Timu ya Kazibizyo Fc nao pia wakipokea zawadi ya mshindi wa Pili Ligi ya Doto Cup kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko.

  Timu ya Uyovu Fc wakipokea zawadi ya mshindi wa kwanza Pamoja na Kombe la  Ligi ya Doto Cup kutoka kwa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko katika viwanja vya Kilimahewa Mjini Ushirombo.

 Baada ya michuano ya Ligi ya Doto Cup iliyofanyika katika Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita  kuanzia ngazi za Vijiji,Kata,Tarafa na hatimaye Wilaya na kila ngazi ikijinyakulia Zawadi kwa kila hatua, Timu ya Uyovu Fc iliyopo  Kata ya Uyovu, Tarafa ya Siloka  jana imejinyakulia  zawadi ya chezi pea tatu,kitita cha shilingi Laki mbili na mpira moja baada ya kuichapa gori 3-0 Timu ya Kazibizyo Fc katika hatua ya fainali ngazi ya Wilaya  iliyohitimisha hapo jana katika uwanja wa Halmashauri ya Bukombe iliyopo eneo la Kilimahewa.

 Huku nafasi ya mshindi wa pili ikishikiliwa na  timu ya Kazibizyo Fc na kufanikiwa kunyakuwa zawadi ya  Jezi pea mbili mpira mmoja na kiasi cha Tsh Laki mbili na nafasi ya mshindi wa tatu ikikaliwa na timu ya Namsega Fc  baada ya kuichapa gori 1-0 timu ya Buntubili Fc  mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika hatua ya fainali hiyo iliyohudhuria na mamia ya mashabiki Timu ya Uyovu Fc ilijipatia gori la kwanza dhidi ya Timu ya Kazibizyo Fc dakika 1,dakika ya 5 gori la pili na dakika ya 20 gori la tatu kupitia kwa kiungo mshambuliaji Deonatus Mkumbulo ‘Ndaki’.

Hadi dakika ya tisini ya mchezo huo Timu ya Kazibizyo Fc haikupata hata gori la kufutia chozi.

 Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi, Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko amezipongeza timu zote zilizojitokeza kushiliki ligi hiyo  kusema atakuwa akiandaa Ligi kama hiyo kwa kila mwaka ili kuhakikisha anaendeleza vipaji vya vijana wanaopatikana ndani ya jimbo la Bukombe waweze kufika mbali na kuiwakilisha Wilaya ya Bukombe kimchezo.   


Comments