CCM MKOA-GEITA: HAKUNA UMWAPA,HAKUNA MADENI YA PEMBEJEO


Kamati ya Siasa ya Halmashauri kuu ya CCM Mkoa wa Geita imesema wakulima wa Pamba Mkoani hapa hawawajibiki kulipa madeni ya Pembejeo waliyokopeshwa na UMWAPA, kwa sababu pembejeo hizo hazikuwa na ubora na zimewasababishia hasara kubwa wakulima wa pamba.

Akizungumza Katibu wa siasa na uenezi CCM Mkoa wa Geita Bwn. Said Kalidushi amesema  hayo alipokuwa akiongea ya Blogu ya Bukombe sasa kuwa hayo ni maamuzi yaliyofikiwa kwenye kikao hicho na kwamba wameitaka Serikali kutoa maelekezo hayo haraka kwenye ngazi za Wilaya ili wakulima wasiibiwe tena.
‘UMWAPA haitakiwi  Mkoa wa Geita kwani wananchi walitarajiwa kulipwa fidia kutokana na mbegu na madawa yaliyosambazwa na UMWAPA kukosa ubora kabisa ‘ Alisema Bwn. Kalidushi. 

Msimu uliyopita pembejeo zilizo sambazwa kwa wakulima hazikuwa na ubora kwani mbegu zilizosambazwa hazikuota kwa kiwango cha kuridhisha na madawa ya kuuwa wadudu hazikuwaua  jambo  ambalo limefanya uzalishaji  wa zao la Pamba kushuka sana huku wakulima wakipata hasara kubwa na kuyumba kiuchumi.
Pamoja na kuwepo kwa hali hiyo bado wanunuzi wa Pamba wakalazimika kudai madeni toka kwa wakulima ambao walisababishiwa hasara kubwa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Bwn. Mashaka Kasoga,Rashid Mstafa na Samagwa Daniel wame kishukuru sana Chama cha Mapinduzi (CCM) kwa hatua walizo zichukua dhidi yao ya kuwatetea watu wanyonge kwa kuwapunguzia adha ya kudaiwa.

Katika hatua nyingine Bwn. Kasoga amewaomba wakulima wenzake kushirikiana na serikali kwa pamoja ili  kuhakikisha kilimo cha Mkataba baina ya wakulima na mawakala wanao kukopesha pembejeo za kilimo  na matokeo yake kupewa pembejeo zisizo na ubora kabisa wasijitokeze tena.

Comments