Wananchi wa Namparahara-Bukombe waungwa mkono na Wawakilishi wao katika maendeleo


Wananchi wa Kijiji cha Nampalahara wakimpokea Mbunge wao Mhe.  Doto Mashaka Biteko na Diwani wa Kata ya Busonzo Mhe. Nikas Mayala

Diwani wa Kata ya Busonzo Mhe. Safari Nikas Mayala akizungumza na wananchi wa Kata hiyo


Picha ya baadhi ya waliyouliza maswali kwenye mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko katika Kijiji cha Namparahara Kata ya Busonzo.

Baadhi ya wananchi wakimsikiliza Mbunge wao Mhe Doto Mashaka Biteko katika mkutano uliofanyika katika kiwanja cha Gengeni - Namparahala
 
Wananchi wa Kata ya Busonzo Wilayani ya Bukombe  wamemuomba Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kuwasaidia kuihimiza serikali ili iwaletee miradi ya visima virefu kwani adha ya huduma ya maji ni kubwa mno.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya  wananchi hao bi Matha Petro na Bw Emanuel Philip  wamesema kuwa  wamekuwa wakiteseka sana kupata maji hasa wakati wa kiangazi kwani visima walivyonanyo ni vya muda mfupi (wakati wa masika)na vingine ni visima vivilivyochimbwa kina kifupi na kuwa na uchache wa maji.
Katika hatua nyingine bw Emanuel Philip amemuomba Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kuwasaidia kupata Kituo cha Afya na Shule kwani watoto wao wamekuwa wakienda mbali kupata elimu na kutokufika kwa wakati na wengine hata kukata tamaa ya kuendelea na masomo.
Pia Diwani wa Kata ya Busonzo Mhe. Safari Nikas Mayala amewataka wananchi hao kuachana na maswala ya kisiasa na kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mbunge wao Mhe. Doto Mashaka Biteko ili kuendelea kufanya maendeleo ya pamoja kwa maslahi ya Kata, Wilaya na  nchi kwa ujumla.
Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko  ameahidi kushirikiana na serikali katika ujenzi wa Barabara ya Uyovu- Bwanga iliyokuwa imekwama kwa mda wa miaka mitatu bila mafanikio hivyo kuwashauri wananchi kuendelea kujishughulisha na miradi ya maendeleo kwa ajili ya kujiimarisha kiuchumi.
Katika hatua nyingine Diwani wa Kata ya Busonzo Mhe. Safari Nikas Mayala  ametoa shilingi laki tano na   Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko ametoa mifuko hamsini ya sementi ikiwa ni juhudi za kuwaunga mkono wananchi katika ujenzi wa shule ya msingi Gengeni iliyoko Kijiji cha Namparahara.

Comments