Mbunge Doto akutana na wananchi wa Kata ya Lyambamgongo

 Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisaini kwenye kitabu cha wageni Lyambamgongo.

 Diwani wa Kata ya Lyambamgongo Mhe. Boniphace Shitobelo akizungumza na wananchi wa Kata yake   

 Mtumishi wa  Mungu akifanya maombi kwa ajili ya ufunguzi wa Mkutano

  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi wa Lyambamgongo katika mkutano wa hadhara.


Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe,Doto Mashaka Biteko amefanya ziara katika Kijiji cha Lyambamgongo, Kata ya Lyambamgongo, Tarafa ya Bukombe Wilayani Bukombe na kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji hicho.
Katika mkutano huo Mhe, Doto Biteko(Mb) amewashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa mwakilishi wao na kuahidi kutowaangusha na kusema atawasilisha Bungeni yale watakayo sema wananchi na sio mawazo yake hivyo wamuunge mkono na kumuombea. 
Aidha katika mkutano huo wananchi waliorodhesha changamoto zao ikiwa ni miundo mbinu duni ya barabara,ukosefu wa kituo cha afya,ukosefu wa malisho ya mifugo yao na kucheleweshewa pembejeo za kilimo hali inayowakwamisha katika uzalishaji  bidhaa zinazotokana na kilimo cha mazao na kusababisha uchumi wao kuyumba.
 Aidha Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Biteko amewaomba wananchi wajitahidi kuwahudumia watoto wao kwa kuwanunulia vifaa vya shule kwa wakati ili kushirikiana na serikali inayotoa elimu bure  na kuwasihi wananchi hao kuachana na siasa za kukwamisha  maendeleo na kuwaambia wafanye kazi  kwa kushirikiana na viongozi wao bila kujali itikadi zao dini wala ukabila kwani Tanzania ni moja na wakati wa siasa sio huu.  



Comments