Wachezaji wakiwa uwanjani
Picha ya kamati ya usimamizi wa michezo kati ya Busonzo
Picha ya anae husika na huduma ya kwanza
Wachezaji wakiwa na mashabiki kwa pamoja wakisubiri hatua ya utoaji wa zawadi
Afisa Mtendaji wa Kata ya Busonzo Bw Shitwala Lukuba akitoa zawadi kwa mshindi.
Mechi hiyo iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki katika uwanja
wa Namparahara Timu ya Narusunguti ilichapa gori 1 Timu ya Mtunduni Fc dakika
ya 42 kupitia kwa kiungo mshambuliaji Nyorobi
Benard.
Hadi dakika tisini ya mchezo huo Timu ya Mtunduni fc
haikupata hata gori la kufutia chozi.
Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi, Afisa Mtendaji wa Kata ya Busonzo Bw Shitwala
Lukuba amezipongeza timu zote zilizojitokeza kushiliki ligi hiyo iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe
Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa lengo la kuendeleza vipaji vya vijana wanaopatikana ndani
ya jimbo la Bukombe.
Katika finali hiyo Timu ya Narusunguti Fc iliibuka na zawadi
ya mshindi wa kwanza kwa kupata mpira 1
pamoja na kiasi cha shilingi elfu
hamsini huku Timu ya Mtunduni Fc ikipata
zawadi ya mshindi wa pili kwa kupata mpira moja.
Kwa upande wake kocha wa timu ya Mtunduni Fc Bw Burugu Yeyema
ameshukuru kwa timu yake kupata nafasi ya pili katika ligi hiyo na kuwataka
wachezaji wa timu yake kutokata tamaaa kutokana na kusindwa kufikia malengo waliyokuwa wamejiwekea ya kushika nafasi ya kwanza na kunyakuwa zawadi
hiyo nono na kuwasihi wachezaji wake
kuendelea kufanya mazoezi kwa bidii ili kuendeleza vipaji vyao.
Nae kocha wa timu ya wa timu ya Narusunguti Bw Yohana Tomasi
amewashukuru wachezaji wake kwa ushindi walioupata na kuwataka kuendelea
kufanya mazoezi kwa bidii ili
kufika hatua ya finali ngazi ya
wilaya.
Aidha baadhi ya mashabiki waliokuwepo uwanjani hapo Joseph
Makoba na Mariamu Mitinje wamekishukuru chama cha mpira wilayani hapa kwa kusimamia vizuri ligi ya doto cup ngazi
ya vijiji na kuwataka kuendelea kuboresha ligi hiyo katika ngazi ya kata,
tarafa na wilaya kwa kuweka waamuzi wenye
sifa zinazokubalika ili kutenda haki
katika ngazi zote.
Comments
Post a Comment