Shekhe wa msikiti
wa wamasijid Nuru Ushirombo Ostadhi
Abudman Yasini akitoa mawaidha katika viwanja vya Bulangwa wakati wa Eid El Fitri
Kaimu shekhe wa Wilaya Ally Jumapili akizungumza na waumini wa wa dini ya kiislamu wakati wa ibada ya Eid El Fitri
Wamama wa kiislam wakisikiliza mawaidha katika viwanja vya Bulangwa wakati ibada ya Eid El Fitri
Picha ya pamoja ya viongozi wa dhehebu la kiislamu Wilayani Bukombe baada ya ibada ya Eid El Fitri
Kaimu shekhe wa Wilaya Ally Jumapili akizungumza na waumini wa wa dini ya kiislamu wakati wa ibada ya Eid El Fitri
Waumini wakijiandaa kwa kutoa swadaka
Wamama wa kiislam wakisikiliza mawaidha katika viwanja vya Bulangwa wakati ibada ya Eid El Fitri
Picha ya pamoja ya viongozi wa dhehebu la kiislamu Wilayani Bukombe baada ya ibada ya Eid El Fitri
Waumini wa dini ya kiislamu Wilayani Bukombe Mkoani Geita,
wamehimizwa kuendelea kudumu katika imani ya kiislamu wakati wote na kusimamia
mafundisho waliyoyapata wakati wa mwenzi mtukufu wa ramadhani.
Akizungumza katika ibada ya Eid El Fitri Shekhe wa Msikiti
wa Masijid Nuru Ushirombo Ostadhi
Abudman Yasini amewataka waiislamu kudumu katika imani hasa katika mafundisho
waliyoyapata katika mwezi huu mtukufu wa ramadhani na kuendelea kujitenga na
mambo yasiyompendeza mwenyezi mungu
wakati wote
Amewataka waislamu kuendeleza upendo na kuwa wakarimu kama
wanavyoelekezwa na viongozi wao kwa kuwasidia wasiojiweza katika kupata
mahitaji muhimu katika maisha yao.
Kwa upande wake Kaimu Shekhe wa Wilaya Ally Jumapili
amewataka waumini wa dini hiyo kuendelea kufanya kazi zao kwa uaminifu na
uadilifu na bila dhuluma kwa kuwa dini inakataza mdhuluma kwa mwiislamu na kupenda kufanya kazi za kuwaingizia kipato
kwa njia halali ili kuendelea kujenga uchumi
wa nchi ya Tanzania na kuacha matendo
yasiyo mpendeza mwenyezi mungu.
Comments
Post a Comment