Mbunge Doto afanya ziara Kata ya Runzewe Magharibi



 Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akisalimiana na baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Msangila kabla ya kuelekea mkutanoni

  Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza  na wanafunzi wa Shule ya Msingi Msangila baada ya kufika mkutanoni hapo wakiwa wamebeba mabango

 Picha ya baadhi ya wananchi wa Kijiji cha Msangila wakimsikiliza Mbunge wao
Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe,Doto Mashaka Biteko amefanya ziara katika Kijiji cha Msangila, Kata ya Runzewe Magharibi, Tarafa ya Siloka Wilayani Bukombe na kufanya mkutano wa hadhara katika Kijiji hicho.
Katika mkutano huo Mhe, Doto Biteko(Mb) amewashukuru wananchi kwa kumchagua na kukubali kujitokeza katika mkutano huo ili kujadiliana mustakabali wa maendeleo na changamoto za eneo hilo.
Aidha katika mkutano huo wananchi waliorodhesha changamoto zao ikiwa ni ukosefu wa pembejeo,miundo mbinu duni ya barabara,ukosefu wa kituo cha afya,ukosefu wa malisho ya mifugo yao,kutafutiwa soko la mazao yao hasa udaga na kuomba kuimarishiwa ulinzi na usalama ndani ya kata hiyo
Katika hatua nyingine wanafunzi wa Shule ya msingi Msangila iliyoko Kata hiyo wameandama hadi  kwenye mkutano wa hadhara wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe, Doto Mashaka Biteko wakiomba kutatuliwa  changamoto zinazowakabili  ikiwemo ukosefu wa vifaa ya michezo, hali inayowafanya kushindwa kushiliki michezo shuleni .
Wakizungumza na blog ya Bukombe sasa wameiomba serikali  kuwajengea visima vya maji, , vyoo, walimu wa kutosha kutokana na uhaba mkubwa wa walimu walionao na madawati hali inayowafanya wanafunzi zaidi ya 120 kukaa chini .
Wanafunzi hao waliokuwa wamebeba mabango yaliyoandikwa


 Aidha Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Biteko amesema atashirikiana na wananchi hao kwa karibu kuhakikisha wanamaliza changamoto zao na kama si kuzipunguza na kuahidi kuwapatia wanafunzi hao vifaa vya michezo ikiwemo seti ya jezi za wasichana na wavulana, mipira na nyavu kwa ajiri ya kushiriki michezo wawapo shuleni.

Comments