BASI YA FALCON YATELEKEZA ABIRIA STENDI USHIROMBO

Abiria wakishauliana la kufanya baada kutelekezwa

Hali halisi ya abiria hao baada ya safari kukwama

Askari Polisi akiwasikliza abiria hao

Basi ya Kampuni ya Falcon yenye namba za usajiri T415 DCJ inayo fanya safari zake  Bukomba -  Dar Es Salaam imetelekeza abiria wake 60 katika stendi ya mabasi mjini Ushirombo Wilayani Bukombe Mkoani Geita, Dereva, kondakta na tingo kuwakimbia watejawao bila ya taarifa.
 
Wakizungumuza kwa nyakati tofauti abiria hao Hames Issa mwenye tiketi yenye namba 145873 amesema safari ya kutoka Dar Es Salaam stendi Ubungo  iliaza jana Julai 17 majira ya saa 12:00 asubuhi lakini kufika Gairo walitumia masaa tisa Dodoma, Singida walifika saa 8:00 usiku hali ambayo siyo ya kawaida.

Issa amesema Julai 18 majira ya saa 5:00 asubuhi tuliigia Ushirombo wakati wakiwa ushirombo Kondakta wa bas hilo aliwaomba kuwa wavumilivu  gari tangu jana linatatizo lakini cha kushangaza hadi saa 8:00 mchana hatuoni hata mmoja wamekimbia kusiko julikana
.
Abiria mwenjiristi wa kanisa la (SDA) Sevet dey Advetntista wasabato Siaberth Terugwa mwenye tiketi namba 145202 amesema amelipa nauri harali Sh 60,000 kutoka Dar Es Salaam hadi Bukoba alikuwa anaenda kwenye msiba akisubiliwa nyumbani kwa ajiri ya mazishi ya  dada yake katika kijiji cha Kasharu kata ya Kasharu Wilaya ya Bukoba vijiji  Mkoani Kagera.

Terugwa alitaja changamoto aliyoipata baada ya kukimbiwa na Dereva,Kondakta na taniboi  kutojulikana waliko kwenda nakwamba kibaya zaidi hata fika kwenye mazishi ya ndugu yake na tayali amesha luhusu mazishi yaendele kutokana na changamoto hiyo aliomba serikali kuingiria kati ili gari hilo liweze kuwafikisha wanako kwenda lakini kutokana kutoelewana vizuriabilia wameingiwa  hofu na wasiwasi yakutokufika salama Bukoba hivyo serikali iliagalie na isimamie warudishiwe nauri zao na watafute basi jingine la kuwafikisha Bukoba.

Meneja wa usafirishaji wa kampuni ya Falcon yenye tin: 104-443-249 Rovikoki Maro  amesema amepata taarifa za basi kuhalibika kutoka kwa abiria lakini anajalibu kutafuta mawasiliano ya Dereva na Kodakta hawapatikani lakini tagu jana wakiwa Morogoro wamekaribia Dodoma lilitokea tatizo la mfumo wa gia lakini aliwasiliana nao na tatizo lili patiwa ufumbuzi na safari iliendelea.

Maro amesema kuhalibika kwa basi Ushirombo Wilayani Bukombe hajapata taarifa na kwamba anafanya mawasiliano na Dereva na Kondakta bila mafanikio  ili kama kunatatizo kubwa afanye mawasiliano ya kuagiza Basi Jingine la kampuni yao ya Falcon zilizopo Geita ili ichukue abilia waendele na safari ya kwenda Bukoba.

Kamanda wa polisi Mkoa wa Geita Mponjoli Mwabulambo simu yake ya mkononi ilipokelewa na walinzi wake na kusema kuwa yuko kwenye kikao lakini awali polisi Wilaya ya Bukombe wamefika stendi na kuthibitisha changamoto za abilia na kwamba Wanawatafuta Dereva na Kodakta wa basi hilo ili kuhakikisha wanaendelea na safari yao.

Comments