Ziara ya kwanza ya Mkuu mpya wa Wilaya ya Bukombe



 Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Josephat Maganga(mwenye suti katikati) na kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya pamoja na Daktari wa Kituo cha Afya Uyovu (mwenye koti jeupe)wakielekea kwenye mradi wa ujenzi wodi ya wazazi itakayofunguliwa na mwenge wa uhuru.

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe Mkoani Geita Josephat Maganga ameanza ziara yake ya kwanza katika Tarafa ya Siloka Wilayani Bukombe kwa kutembelea  miradi mbalimbali ya maendeleo  itakayozinduliwa na kuwekewa jiwe la msingi  julai 31 mwaka huu.
Bw Maganga ametembelea katika Kituo cha Afya cha Uyovu kukagua mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji (Theater)unaofadhiliwa na shirika la umoja wa mataifa linalohusika na idadi ya watu(UNFPA) na ugawaji wa vyandaruwa vyenye dawa, mradi wa ujezi wa Barabara ya Uyovu, Kabagole na Nakayenze, Mradi wa ujenzi wa soko la mazao ya biashara Namonge, Vyumba vya Madarasa na Nyumba za walimu (six in one) katika shule ya sekondari Namonge na ujenzi wa josho la kuogeshea ng’ombe katika Kijiji cha Msonga.
                           
 Picha ya miradi iliyokaguliwa wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya Bukombe 
Mradi wa ujenzi wa wodi ya wazazi na chumba cha upasuaji (Theater)unaofadhiliwa na shirika la umoja wa mataifa linalohusika na idadi ya watu(UNFPA) katika Kituo cha Afya Uyovu.

   Mradi wa ujenzi wa Barabara ya Uyovu, Kabagole na Nakayenze

Mkuu wa Wilaya ya Bukombe na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya wakikagua Mradi wa ujenzi wa soko la mazao ya biashara Namonge
 
  Nyumba za walimu (six in one) katika shule ya sekondari Namonge

Katika ziara hiyo mkuu wa Wilaya Josephat Maganga  ameambatana na baadhi ya wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama kumtambulisha kwa wakazi wa maeneo ya Tarafa ya Siloka na kujua vipaumbele vyao katika kusukuma maendeleo ya Wilaya ya Bukombe.     
Moja ya vibaumbele vya wananchi hao kwa Mkuu wa Wilaya Josephat Maganga  ni kuendelea kujenga umoja wa wananchi, kuboresha sekta ya kilimo cha mazao ya biashara na chakula kwa kutoa pembejeo za kilimo kwa wakati, kuboresha sekta ya elimu kwa kwa kuhimiza serikali kujenga vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, madawati na mabweni kwa wanafunzi wa kutwa, na kuboresha sekta ya afya hasa kujenga vituo vya afya katika kila kata ili kuokoa vifo visivyo vya razima kwa kutembea mwendo mrefu kutafuta matibabu. 
 Aidha kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Bukombe amesema atahakikisha anatoa ushirikiano wa kutosha kwa wananchi hao hasa katika maswala ya kuiweka wilaya hiyo kuwa salama na kuhimiza maendeleo kwa wananchi na kuwataka viongozi walio katika ngazi za Tarafa, Kata ,Vijiji na Vitongoji kutenda haki na kusimamia ukweli  kwa maslahi ya Wilaya na Taifa kwa ujumla.


Comments