Timu ya
Ituga fc imeichapa gori 1-0 timu ya Lyambamgongo fc katika ufunguzi wa Ligi
ya Doto Cup ngazi ya Tarafa iliyofanyika katika uwanja wa Kijiji cha Bukombe Tarafa ya Bukombe Wilayani Bukombe
mkoani Geita.
Mechi hiyo
iliyohudhuliwa na mamia ya mashabiki,timu ya Ituga fc ilijipatia gori dakika ya
25 ya kipindi cha kwanza kupitia kwa Jofrey Maiga, hadi dakika 90 timu ya Lyambamgongo haikupata hata gori la kufutia chozi.
Akizungumza
wakati wa ufunguzi wa ligi ya Doto Cup ngazi ya Tarafa katibu wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe ndugu Benjamini Mgeta amesema Ligi hiyo ni kwa ajili ya kukuza
na kuinua vipaji ya vijana Wilyani hapa na kuwataka wachezaji wanaoshiriki Ligi
kufanya mazoezi zaidi kabla ya kushiriki mechi ili kujiweka sawa katika
kunyakuwa zawadi ya mshindi wa kwanza ngazi ya Wilaya.
Kwa upande
wake mwenyekiti wa Chama cha Mpira Wilayani hapa bw Peter Bomani amesema
atahakikisha haki inatendeka kwa kila timu inayoshiriki Ligi hiyo na kwamba
atasimamia vyema sheria na kanuni za
mpira wa miguu ili kupata timu bora ya Wilaya kupitia Ligi ya Doto Cup.
Comments
Post a Comment