Wafugaji wa Wilaya ya Bukombe wakutana na Mbunge wao

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko(aliyesimama) akizungumza na baadhi ya wafugaji wa Wilaya ya Bukombe katika ukumbi wa Shule ya Sekondari Runzewe.

Baadhi ya Wafugaji wa Wilaya ya Bukombe waliojitokeza kushiriki katika kikao cha ndani cha Wafugaji katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Runzewe 

Wafugaji wa Wilayani Bukombe Mkoani Geita, wamehimizwa kuendelea kudumu katika umoja na ushirikiano wakati wote na kusimamia ukweli ili kuepusha migogoro isiyo ya lazima katika jamii inayowazunguka.
Akizungumza katika kikao hicho Diwani wa Kata ya Busonzo na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Bukombe Mhe. Nikas Mayala Safari amesema kila hatua inagharama zake na kuwaomba wafugaji wasivunjike moyo katika suala zima la ufugaji kwani ipo siku jambo la malisho ya mifugo yao litapatiwa mwafaka wake.
Pia mwenyekiti wa Chama cha wafugaji  Kanda ya Ziwa(CHAWAKAZI) Bw. Juvenari Mlashani amewataka wafugaji wote kushiriki kikamilifu katika huduma za kijamii bila kujali itikadi, dini wala ukabila ili kujiletea maendeleo kwa haraka na kuimarisha uchumi wao na nchi kwa ujumla.

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko  ameanza kwa kuwapa pole wafugaji kwa misukosuko yote iliyojitokeza na kuwataka wafugaji kutokata tamaa ya kuendelea kufuga na kuwasihi kuzidi  kushikamana kwa pamoja wao kwa wao na kushikiana na serikali ili kuharakisha mafanikio na kuwaomba wawe tayari kubadilika kwenda kwenye ufugaji wa kisasa kilingana mifugo kuzidi kuongezeka na ikiwa eneo ni  lilelile .  


Comments