Mbunge Doto afanya ziara katika Kata mbili




 Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko na Diwani wa Kata ya Katome Mhe. Paul Mhangwa wakibadilishana mawazo kabla ya mkutano kuanza.
  Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi wa kata ya Igulwa.

Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mkoani Geita Mhe,Doto Mashaka Biteko amefanya ziara katika Kata mbili za Katome na Igulwa  Wilayani Bukombe na kufanya mikutano ya hadhara katika Kata hizo.
Katika mikutano hiyo Mhe, Doto Biteko(Mb) amewashukuru wananchi kwa kumchagua kuwa Mbunge wao na kuwasihi wananchi hao kuachana na itikadi za vyama dini na ukabila kwa wakati huu na badala yake kila mwananchi ashirikiane na viongozi walioko madarakani  kwa pamoja  kuleta maendeleo katika Wilaya yao ya Bukombe.
Aidha katika mikutano hiyo wananchi waliorodhesha changamoto zao huku wakianzia Kata ya Katome kwa kusema changamoto zao ni kutozwa pesa kwenye huduma za afya za mama na mtoto,ukosefu wa visima virefu,pembejeo kutokufika kwa wakati  na unyonywaji wa wakulima kwa wafanya biashara wa  mazao kwa kuwapimia kwenye kipimo kisicho sahihi(Mozambiki) 

Wananchi wa Kata ya Katome wakimsikiliza Doto Mashaka Biteko (Mb)
katika mkutano uliofanyika katika kijiji cha Bugama  
Katika upande wa Kata ya Igulwa wamesema changamoto zao ni ukosefu wa miundo mbinu ya barabara,huduma ya maji safi,kukosa choo cha wanafunzi shuleni,kituo cha afya,wingi wa wanafunzi shuleni na waalimu ni wachache,vifo vya wachimbaji wadogo kwa kukosa vifaa vya kisasa vya kuchimbia madini na migogoro ya wafugaji na wakulima kugombania maeneo ya kuchungia
 Wananchi wa Kata ya Igulwa wakimsikiliza Doto Mashaka Biteko (Mb)
 katika mkutano uliofanyika katika kijiji cha Buntubili
 
Akizungumza kwa nyakati tofauti  kwenye mikutano hiyo amasema kuwa atahakikisha anashirikiana na serikali ili umeme vijijini uwenee kwa wingi kwa kuviingiza vijiji hivyo kwenye mpango wa umeme vijijini REA na kuongeza mawasiliano ya barabara zinazounganisha maeneo mbalimbali hususani kijiji na kijiji, kata na kata na hata wilaya na wilaya kwa kuziingiza kwenye mfuko wa TANROAD baadhi ya barabara hizo na kuwaomba wananchi hao kujitoa kwa dhati kwenye shughuli zozote za maendeleo.

Comments