Halmashauri kuu ya CCM yapewa taarifa ya utendaji ya miezi sita

Mbunge wa jimbo la Bukombe Mhe Doto Biteko(aliyesimama) akizungumza na Halmashauri ya CCM ya Wilaya ya Bukombe.

Moja ya mumbe akichangia mada


Taarifa ya utendaji wa Mbunge wa Jimbo la Bukombe ameitoa kama ifuatavyo

 OFISI YA MBUNGE JIMBO LA BUKOMBE
TAARIFA YA UTENDAJI KWA HALMASHAURI KUU YA CCM YA WILAYA, KATIKA KIPINDI CHA NOV 2015- JUNE,2016
10/7/2016.
1.Utangulizi
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama unavyofahamu ofisi yako ilisimamia vema uchaguzi wa mwaka 2015. Juhudi zako na ofisi yako ziliniwezesha kuchaguliwa kuwa mbunge wa jimbo la Bukombe.
Naomba nikushukuru sana wewe na watendaji wote wa ofisi yako kwa ushirikiano, miongozo na maelekezo mbalimbali mliyonipatia wakati wote wa kampeni. Maelekezo yenu ndiyo yaliyofanya tushinde vizuri katika uchaguzi huo.
Hata hivyo naomba niombe radhi ikiwa kwa namna moja au nyingine sikufanya vizuri katika kuzingatia maelekezo ya ofisi yako.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya uchaguzi kinachofuata ni kazi. Kazi ya kutekeleza ahadi zote zilizoahidiwa wakati wa kampeni. Aidha ni wakati wa kuisimamia serikali ili itekeleze vyema ilani ya uchaguzi ya CCM kwa kiwango cha kupimika. Kutokana na ukweli huo, mimi kama mbunge nalazimika kutoa taarifa kwa chama na nimejiwekea utaratibu wa kutoa taarifa kila baada ya miezi sita.
2. Mhutasari wa kazi zilizofanyika kwa kipindi cha novemba 2015 –Juni,2016
Tukio
Yaliyofanyika
Matokeo
1.    Uundaji wa ofisi ya mbunge
·         Katibu wa CCM kata ya Uyovu aliteuliwa kuwa katibu wa Mbunge
·         Ofisi ya mbunge kwenye chama ilifunguliwa







  • Uratibu na mawasiliano ya mbunge vimerahisishwa, aidha wana ccm na wananchi wengine watapata nafasi zaidi ya kukutana na mbunge au katibu wake.


Uundaji wa akamati ya mfuko wa jimbo

  • Kamati imeshatarifiwa juu ya uteuzi vikao vitaanza wiki hii. Tsh 53,000,000 zimepokelewa tayari

2.    Ziara
a)    Mikutano ya Hadhara na ya ndani ya CCM
·         Mbunge ametembelea jumla ya kata 16 kati 17
·         Ahadi kadhaa zilitolewa na mbunge
·         Hoja mbali mbali ziliibuliwa na jumla ya maswali zaidi ya 900 yaliulizwa na kufafanuliwa kwenye mikutano hiyo.
·         Ahadi mbalimbali zimeshatekelezwa na nyingine zitakamilishwa mwezi huu.( Angalia kiambatisho na2)
·         Kero mbalimbali zilipatiwa ufumbuzi mf. Uwepo wa ofisi ya TANESCO Bukombe na uongezwaji wa nguzo za umeme kwenye mradi wa electricity iv.
·         Ukarabati wa barabara ya Katoro Ushirombo ushakamilika.
·         Jumla ya madai ya walimu 208 yalishughulikiwa na kurekebishwa kwenye Lawson utumishi
·         Ukaguzi ulifanyika kujua kama kweli fedha 10,000,000/ zilizodaiwa kuibiwa kwenye akaunti ya kijiji Ng’anzo.
·         Vipimo vya Mozambique vimefutwa na maelekezo ya vipimo vya mazao ya nafaka yametolewa.
·         Miradi ya MIVARF imeanza kutekelezwa uyovu na Namonge
·         Mwekezaji Ng’anzo aliahidi kukamilisha ujenzi wa nyumba za walimu na kifusi kilichokua kinaingia kwenye nyumba za watu kimerekebishwa.

b). Kutembelea taasisi
·         Kituo cha afya uyovu kilitembelewa
·         Walimu wa kata ya Runzewe Magharibi walitembelewa
·         Hospitali ya wilaya ilitembelewa
·         Kituo cha polisi Uyovu kilitembelewa
·         Runzewe sekondari

Kero mbalimbali zilitolewa na watumishi wa taasisi hizo na majibu yaltolewa
3.    Maafa/Majanga
·         Kitongoji cha Idoselo nyumba 40 zilichomwa moto na maofisa wa maliasili
·         Familia iliyopata matatizo ya kufariki mama na watoto kwa kula chakula kilichodhaniwa kuwa na sumu
·         Wahanga walitembelewa na mikutano miwili ilifanyika na misaada ya chakula na maturubai vilitolewa.
·         Wafiwa walitembelewa na kupewa mkono wa pole
4.    Mialiko kwa mawaziri
Mialiko hii ni kutokana na uwepo wa changamoto zilizohitaji utatuzi kutoka serikali kuu.
·         Mawaziri jumla ya ziara 6 wa sekta mbalimbali waheshimiwa, (Mwigulu Nchemba, Eg. Ramo Makani, Dr. Medard Kalemani, Prof. Jumanne Maghembe na Hamad Masauni)
walifika na kusaidia kutatua changamoto hizo.
5.    Mikutano
Mikutano mbalimbali ya kazi ilihudhuriwa kuanzia ngazi ya wilaya, mkoa, Taifa na nje ya nchi.
·         Mbunge alihusika katika kutoa maamuzi na aidha kuwakilisha bunge kwenye mikutano nje ya nchi.
6.    Harambee na machangizo mbalimbali
Utoaji wa michango ulifanyika kwenye makanisa mbalimbali na tasisi nyingine
Uimarishaji wa mahusiano na kukuza imani ya wanachi kwa viongozi wao.
7.    Michezo
Vifaa mbalimbali vya michezo vimegawiwa kwa vijana ikiwemo jezi na Mipira.

Ligi ya jimbo imeanza
Michezo imeendelea kufanyika



Ligi inawendelea

3. Kuitambulisha wilaya ya Bukombe.
 Mheshimiwa Mwenyekiti, Ili maendeleo yafike mahali popote lazima kwanza mahali hapo pajulikane. Duniani sehemu kubwa ya fedha za makampuni au taasisi 40% ya mapato yao huenda katika kujitangaza. Na Bukombe inahitaji kujitangaza ndani na nje ya nchi ili kuwavutia wawekezaji katika kushiriki uchumi wetu.
Ili kutekeleza hili blogu maalumu ya Bukombe imeanzishwa iitwayo BUKOMBE SASA na tumeiweka kwenye PLAY STORE ya simu zote. Mtu anaweza kupata taarifa yoyote kupita blogu.
Mheshimiwa mwenyekiti, naomba sote tuitembelee blogu hii kwa anuani ya bukombesasa.blogspot.com  aidha unaweza kuipakua kwenye playstore ya simu yako ikiwa una smart phone.




4. Mafanikio
Mheshimiwa Mwenyekiti,
Katika kipindi hiki cha miezi 6 ya mwanzo yapo mafanikio kadhaa ambayo kwa kweli ofisi yako pia imeshiriki kufanya yatokee.
·         Wananchi kuwa na matarajio chanya na Mbunge wao
·         Seikali ya awamu ya tano imekuwa nyepesi sana tunapo hitaji msaada wake mfano mmeona  kila tunapoarika mawaziri wanakuja kwa haraka kutusikiliza na kutatua changamoto zetu kwa kiasi kikubwa.
·         Misaada na huduma mbali mbali kwa uchache zimetolewa kwa wananchi kama inavyoonyeshwa kwenye kiamabtisho na 2.
·         Kwa kushirikiana na mbunge wa Mbongwe tunashawishi kupandisha  daraja barabara itokayo ushirombo – Katome- Mbongwe- Bukoli
·         Aidha kwa kushirikiana na Mbunge wa Chato tunashawishi kufungua barabara ya kutokea Kakoyoyo kwenda Bwanga kupitia Nyikonga.
·         Tumefanikiwa kupata madawati ya 400 toka Tamisemi ambayo yamegawanywa kwenye shule 10.
·         Tumekubaliwa na wizara ya mambo ya ndani kupata gari moja kwaajili ya kituo cha polisi uyovu. Aidha tunatarajia kufungua kituo kidogo cha polisi Namonge
·         Miradi ya MIVARF hatimaye imeanza kutekelezwa kwa kujenga soko la kisasa huko Namonge na barabara ya kabagole.
·         Wanafuzi na walimu wa uyovu sekondari walipewa zawadi kwa kufanya vizuri kitaaluma.
·         Kuingiza vijiji vyote kwenye mradi wa umeme vijijini
·         Kuanzishwa kwa ofisi ndogo za TANESCO Bukombe.
·         Kuanzisha ligi ya jimbo kama ilivyoahidiwa wakati wa kamapeni.
·         Tumeingiza kwenye miradi ya maji mwaka huu wa fedha vijiji 10
5. Changamoto
Mheshimiwa mwenyekiti, naomba nilete changamoto chache zinazoikabili ofisi ya mbunge. Changamoto hizi tunaweza kwa pamoja kuzipunguza kama siyo kuzimaliza kabisa. Zifuatazo ni changamoto chache:
·         Upatikanaji wa fedha za miradi kwa wakati imekua ngumu kidogo. Mfano mwaka tuanomalizia ni 26% tu ya fedha za miradi zilipelekwa
·         Jimbo la bukombe limeaminishwa na wanasiasa kuwa wananchi wanapaswa kufanyiwa kila kitu na serikali  jambo ambalo si sahihi.
·         Uwepo wa zahanati chache na vituo vya afya vichache vimefanya utoaji wa huduma za afya kuwa ngumu kwa watoa huduma

6. Hitimisho

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nihitimishe tena kwa kukushukuru wewe na kamati yako ya siasa na halmashauri kuu ya wilaya ya ccm kwa kukubali kunitengea muda huu ili kupokea taarifa yangu. Taarifa ni mhtasari tu wa mambo mengi yaliyofanyika kwa kipindi cha miezi 6.

Ninaomba sasa taarifa hii ipokelewe na kujadiliwa.



Imetayarishwa na:
Doto Biteko (MB)
Mbunge jimbo la Bukombe


NAOMBA KUWASILISHA



Kiambatisho
Mgawanyo wa fedha za mfuko wa Jimbo
1.    Madawati         10,000,000/
2.     Uendeshaji        2,000,000/
3.    CHF                      8,500,000/
4.    Choo Kilimahewa  1,700,000/
5.    Kidete s/m              5,000,000/
6.    Bugama S/M           5,000,000/
7.    Wazee                          500,000/
8.    Ushirombo S/M       3,000,000/
9.    Kapwani S/M            1,500,000/
10. Msonga Sekondari    3,000,000/
11. Bulega Sekondari       3,000,000/
12. Bulangwa S/M             2,000,000/
13. Choo Nyamakunkwa   2,000,000/
14. Buntambala S/M          3,000,000/
15. Choo Busonzo S/M       3,000,000/

















Comments