Ikuzi fc yafanya kweli katika uwanja wa Msonga

Timu ya Bulama fc wakiwa na moja wa kiongozi wao kabla ya kianza mchezo

Picha ya pamoja ya timu ya Ikuzi fc

Wachezaji wa Timu ya Ikuzi fc wakifanya mazoezi kabla ya mchezo kuanza

Kamati ya usimamizi wa Ligi ya Doto Cup Kata ya Runzewe Mashariki wakiwakagua wachezaji kabla ya kuanza kwa mchezo kwenye kiwanja cha Msonga

Kiongozi wa Timu ya Bulama fc ambae ni mshindi wa pili katika fainali hiyo akionyosha zawadi  kwa mashabiki wake 

Picha ya pamoja ya  viongozi wa kamati ya Ligi ya Doto Cup na Timu ya Ikuzi fc iliyochukua ubingwa wakionyesha zawadi kwa mashabiki wao

Picha ya pamoja kwa timu zote zilizoshiriki fainali wakiwa na Kamati ya Usimamizi wa Ligi ya Doto Cup  Kata ya Runzewe Mashariki na washabiki wao



Jana timu ya Ikuzi fc imeichapa gori 2-0 timu ya Bulama fc  katika mchezo wa fainali ya Ligi ya Doto Cup ngazi ya kata uliofanyika katika uwanja wa Msonga uliopo Kata ya Runzewe Mashariki Wilayani Bukombe Mkoani Geita
Mchezo huo uliokuwa wa kushindania zawadi ya kiasi cha shilingi elfu  50 na mpira mmoja kwa mshindi wa kwanza na mshindi wa pili akipata mpira mmoja timu ya Ikuzi fc ilifanikiwa kunyakua zawadi hiyo nono baada ya kuichapa gori 2-0 timu ya Bulama fc 

Gori la kwanza la Timu ya Ikuzi fc imetiwa nyavuni na mchezaji Vitina Kabili dakika ya 18 na   gori la pili na la tatu yamefungwa na kiungo mshambuliaji Yosamu Julius  dakika ya 25  katika kipindi cha kwanza.
Hadi dakika tisini ya mchezo huo Timu ya Bulama fc haikupata hata gori la kufutia chozi.

       
Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi,  Afisa Mtendaji wa Kata ya Runzewe Mashariki Bwana Nestory amezipongeza timu zote zilizojitokeza kushiliki ligi hiyo  iliyoandaliwa na Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko kwa lengo la kuendeleza vipaji vya vijana wanaopatikana ndani ya jimbo la Bukombe . 
  

Comments