MBUNGE WA BUKOMBE ATATUA MGOGORO WA MWEKEZAJI NA WAMILIKI WA MAENEO




Picha ya eneo lenye mgogoro baina ya mwekezaji na wamiliki wa maeneo haya


Mhe. Doto Mashaka Biteko (Mb)(wakatikati),kushoto ni Diwani wa Kata ya Katente Mhe. Bahati Kayagila na kulia ni Kaimu Afisa Madini wa Mkoa wa Geita bwn. Fabian Mshai wakiwa na wananchi wa Kata ya Katente kwenye bicon aliyoweka mwekezaji.


Mchimbaji mdogo akifanya utafiti wa madini


Mbunge wa Jimbo la Bukombe Mhe. Doto Mashaka Biteko akizungumza na wananchi wa Kata ya Ketente.



Picha ya baadhi wananchi wa Kata ya Katente wakimsikiliza Mbunge wao Doto Mashaka Biteko.



.


Wananchi wa Kata ya Katente wakimsindikiza mbunge wao Mhe Doto Mashaka Biteko(katikati) baada ya mkutano nao katika Kata hiyo.




Wananchi wa  Kijiji cha Katente Kata ya Katente Wilayani Bukombe mkoani Geita wameiomba serikali kumaliza mgogoro baina ya wachimbaji wadogo wa madini na mwekezaji  katika eneo hilo kwa kuwapatia suluhu.
Wakizungumza katika mkutano wa Kijiji hicho  na mbunge wa Jimbo la Bukombe mh. Doto Biteko  wakati wakitafuta suluuu ya mgogoro  wamesema kuwa muwekezaji  alivamia maeneo yao kwa madai kuwa ana kutaka kuwekeza katika maeneo yao bila makubalino na wamiliki wa maeneo husika.
wamesema  kuwa maeneo hayo wameyamiliki kwa muda mrefu na kwa kuyatumia katika  shughuli za uchimbaji mdogo, kilimo,ufugaji na makazi.
Kwa upande wake mbunge wa Jimbo la Bukombe Mh. Doto Biteko amesema kuwa serikali ya awamu ya tano haipo kwa ajili ya kuwakandamiza wananchi wa hali ya chiini hivyo lazima muwekezaji yeyote  afuate sheria za uwekezaji.
Katika hatua nyingine Mhe. Biteko  amemuunga  mkono mkuu wa Wilaya ya Bukombe Aman Mwinegoha kwa kitendo cha kusimamisha zoezi la mwekezaji huyo hadi atakapofuata sheria zote za uwekezaji wa madini ili isiwepo migogoro tena.
 Aidha kaimu afisa madini mkoa wa geita bw Fabian mshai amewataka wamiliki wa maeneo kuendeleza shughuli zao za kila siku ikiwemo  kilimo, ufungaji na makazi hadi hapo watakapo maliza migogoro yao baina ya mwekezaji na wamiliki wa maeneo

Comments

Post a Comment