NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI ALIPOFANYA ZIARA KATIKA
JIMBO LA BUKOMBE
Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dr. Medadi Kalemani alipofanya ziara katika jimbo la Bukombe na kuzungumza na wananchi wa jimbo hilo na kuwaahidi kuwapatia wachimbaji wadogo wadogo maeneo ya kuchimba pia kuongeza idadi ya maeneo, kupeleka umeme nafuu Vijiji 53 na Vitongoji 156 hasa kwa wananchi wa kipato cha chini kwa kuwapa chombo kiitwacho Umeme Tayari (UMETA) ili kupunguza gharama za mfumo wa umeme majumbani (wiring).
Picha ya Doto Mashaka Biteko (Mb) akizungumza na wananchi wa Jimbo la Bukombe katika ziara ya Naibu Waziri wa Nishati na Madini Dr. Medadi Kalemani.
Mh. Doto Mashaka Biteko (Mb) na Katibu Tawala Wilaya ya Bukombe wakipokea kifaa kiitwacho Umeme Tayari (UMETA), hiki kinarahisisha uingizaji wa umeme kwenye nyumba bila kuweka mfumo(Wiring).
Comments
Post a Comment