Sentensi za CCM kuhusu uteuzi wa msemaji mpya wa chama aliyechukua nafasi ya Waziri Nape
Ni March 20, 2016 ambapo chama cha
mapinduzi kilifanya mkutano na waandishi wa habari na kumtangaza msemaji
mpya wa chama cha mapindizi baada ya waziri Nape kuteuliwa kufanya kazi
za uwaziri kulitumikia taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari katibu mkuu wa chama hicho, ndugu Abdulrahman Kinana alisema…‘Bw.Christopher
Sendeka yeye sasa ndio atakuwa msemaji wa chama cha mapinduzi kwasababu
gani, kwasababu katibu mwenezi wa chama chetu ndugu Nape
aliteuliwa kuwa waziri wa Serikali na Waziri wa habari utaratibu wa
chama chetu nafikiri ni busara mtendaji wa chama anapoteuliwa kuwa
waziri basi atajishughulisha na kazi yake ya uwaziri lakini kwasababu
katibu mwenezi ameteuliwa na halmashauri kuu ya taifa, uteuzi wake
unateguliwa tu na halmashauri kuu kama alivyoteuliwa na halmashauri ya
kitaifa’ – Kinana
‘Kwahiyo hakuna mwenye mamlaka wa
kutengua uteuzi wake isipokuwa halmashauri ya kitaifa kwahiyo atabaki
kwa jina kuwa mwenezi wa chama chetu mpaka hapo halmashauri kuu
itakapokaa kutengua nafasi hiyo aliyonayo ya mwenezi, lakini tungependa
kazi ya kuisemea chama cha mapinduzi kiendelee kwahiyo tumemteua bwana Christopher Ole Sendeka kuwa msemaji wa chama chetu’ – Kinana chanzo ; Edwini TZA
Comments
Post a Comment